Monday, January 9, 2012

DIAMOND AHUKUMIWA MIEZI SITA JELA



MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Naseeb Abdul (Diamond)


amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela, au kutakiwa kulipa fidia ya

shilingi elfu 80 kwa kosa la kumpiga mwandishi wa habari Mkoani

Iringa.



Hatua hiyo imekuja baada ya msanii Diamond na wacheza shoo wake wawili

kukiri kosa mbele ya mahakama yeye na wenzake kwa kuharibu Camera

mbili, Lap top aina ya Accer pamoja na kumshambulia mwanahabari

Frances Godwin tarehe 31 katika uwanja wa samora mjini hapa.



Akitoa hukumu hiyo hakimu wa Mahakama ya Mwanzo mh.Masua alisema

kulingana na watuhumiwa wote watatu kukiri kosa hilo anawahukumu

kwenda jela miezi 6 au kulipa fidia ya shilingi elfu hamsini kila

mmoja na huku wakilazimika kumlipa Frances shilingi elfu 30 kila

mmoja.



Wakitoa utetezi wao watuhumiwa hao walisema mahakama iwapunguzia

adhabu kwa kuwa hawakukusudia kufanya kosa hilo, na wao walikuja

mkoani hapa kwa ajili ya kutoa burudani, na kuwa tukio hilo

wamelifanya kwa ghadhabu.



Mheshimiwa Hakimu ninaomba unipunguzie adhabu licha ya kutenda kosa

hilo, kwani nakili kuwa nilipatwa na hasira kama binadamu na kuamua

kuchukua uamuzi wa kufanya hayo, mimi sikukusudia kuja Iringa kufanya

vurugu bali hali hiyo ilikuja baada ya kupata ghadhabu kama walivyo

binadamu wengine,” alisema Diamond.



Hukumu hiyo ambayo imezua maswali mengi kwa wanahabari na wananchi

waliohudhulia mwenendo mzima wa kesi hiyo na kuomba vyombo vya sheria

kutenda haki pasipo kuangalia umaalufu wa mtuhumiwa.





Naye mwanasheria Evaristo Myovela alisema kesi hiyo hakimu ametimiza

wajibu wake, huku akimshauri Frances kukata rufaa ili kuipeleka kesi

hiyo katika Mahakama nyingine kwa kufuata utaratibu wa sheria katika

kuchukua maamuzi hayo.



Wakati wanahabari wakijadili juu ya hukumu ya Diamond na jeuri

aliyoonyesha mahakamani hapo, mara Waziri wa nchi sera na uratibu wa

sheria wa bunge Willium Lukuvi alikatiza katika mahakama hiyo ndipo

wanahabari wakataa kupata mawazo na uelewa zaidi juu ya kilichotokea

mahakamani hapo.



Diamond alilipa fidia hiyo na kuachiwa huru licha ya France

kulalamikia mwenendo wa kesi hiyo na kuamua kupeleka barua mahakamani

ya kuomba nakara ya kesi na 13. ya 2012 kwa ajili ya kukata rufafaa.



Hata hivyo chama cha wanahabari mkoani hapa kilimtaka Diamond kufanya

naye maongezi, na yeye kuahidi kufika katika ofisi za Clabu ya

wanahabari (IPC) kwa mazungumzo, jambo ambalo amelikaidi mwanamuziki

huyo


MWISHO

No comments:

Post a Comment