Mgombea wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Bi. Grace Tendega akiwa na mratibu wa CHADEMA nyanda za juu kusini Bw. Frenk Mwaisumbe katika ofisi ya CHADEMA Iringa wakipitia baadhi ya viambatanishi vya Pingamizi la mgombea wa CCM Bw. Godfrey Mgimwa.
Kushoto- Bw. Frenk Mwaisumbe na Bi. Grece Tendega.
Kushoto ni Bw. Godfrey Mgimwa ambaye ni mgombea wa kiti cha Ubunge kwa tiketi ya CCM akitazama "Passpot" yake iliyoshikwa na katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Bw. Hassan Mtenga ikionyesha uthibitisho wa mgombea huyo uzawa na uraia wake wa Tanzania.
"Passport" ya mgombea wa CCM Bw. Godfrey Mgimwa anayelalamikiwa na CHADEMA kuwa si raia wa Tanzania.
Barua ya Godgfrey Mgimwa iliyotoa majibu ya pingamizi lililotolewa dhidi yake na mgombea wa CHADEMA Bi. Grace Tendega, kupinga kushiriki katika kampeni na mchakato wa kuwania kiti cha Ubunge jimbo la kalenga, lililoachwa wazi baada ya Dr. Willium Mgimwa mbunge wa jimbo hilo kufariki dunia mapema Januari 2014.
Passport ya Bw. Godfrey Mgimwa- mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la kalenga- Iringa.
Msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo la kalenga Bi. Pudensiana Kisaka akizungumzia sakata hilo la Pingamizi na hatua zinazoendelea.
Bi. Pudensiana Kisaka.
<<<<<<<<<<<<<<<HABARI>>>>>>>>>>>>
MGOMBEA wa chama cha mapinduzi CCM amebeza pingamizi
lililotolewa na mgombea wa chama cha
demokrasia na maendeleo CHADEMA Bi. Grace Tendega pingamizi lililoitaka tume ya uchaguzi,
kumuengua mgombea wa ubunge kupitia CCM - Godfrey Mgimwa kwa madai ya kutokidhi vigezo vya ushiriki wa uchaguzi huo mdogo
jimbo la kalenga, kikiwemo cha mgombea huyo wa CCM kutokuwa raia halali wa Tanzania.
Akizungumzia hatua ya pingamizi hilo Mgimwa amesema hali hiyo
inaonyesha dhahiri jinsi CHADEMA wanavyohofia ushindi wa CCM na kuwa pingamizi
hilo halina mashiko wala ukweli wowote, huku akiwataka wananchi na wapigakura wa jimbo la Kalenga kuwabeza CHADEMA kwa uzushi huo.
Aidha Mgimwa amesema yeye ni mzaliwa wa mkoa wa Iringa na raia
halali wa Tanzania, na kuwa elimu yake ya msingi kuanzia darasa la kwanza hadi
la saba aliipatia katika shule ya msingi Wilolesi ya mjini Iringa, huku elimu ya
sekondari akisoma shule ya Azania na St.
Mery’s za jijini Dar es salaam.
Aidha Mgimwa amesema kwa kifupi shutuma za CHADEMA siyo za
kweli hata kidogo kwani huku nje ya nchi alikwenda kwa ajili ya kupata elimu ya
chuo cha Uingereza, degree ya miaka mitatu na elimu ya juu kwa mwaka mmoja na
akarudi nchini kwa ajili ya kuijenga nchi kwa kile alichokisomea.
“Ninatoa masikitiko yangu makubwa kwa CHADEMA kwani shutuma
hizo siyo za kweli, kwa ufahamu wangu nchi ya Tanzania hairuhusu mtu mmoja kuwa
na uraia wa nchi mbili, kwani mimi ni raia mzawa halali wa Tanzania na Pasport
yangu hii hapa, wazazi wangu wote niwa Tanzania na nimezaliwa katika Hospitali
ya mkoa wa Iringa, lakini CHADEMA wameshindwa kudhibitisha juu ya shutuma
wanazozielekeza kwangu,” Alisema Mgimwa.
Katibu wa CCM Wilaya ya Iringa Amina Himbo amesema kuhusiana
na Stakabadhi za wadhamini wa Mgimwa hilo sila ukweli kwani wadhamini wa
mgombea wao ni viongozi wa jimbo la kalenga, na wanachama wa CCM wa jimbo la Kalenga
na kuwa pingamizi hilo nila uongo nala hila lenye kutaka kuwadanyanya
wapigakura wa Kalenga.
Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Hassan Mtenga ameitaka CHADEMA kutafuta mbinu nyingine za kuwadanganya wananchi wa kalenga kwa madai kuwa mgombea wao ni Mtanzania na hana dosari yoyote inayomfanya asishiriki uchaguzi huo mdogo wa jimbo la kalenga.
Akizungumzia juu ya pingamizi lake mgombea wa CHADEMA Grace
Tendega amesema anachopinga si uraia pekee ndiyo ameuwekea pingamizi dhidi ya mgombea wa
CCM Mgimwa, bali hata baadhi ya wadhamini wa Mgimwa shahada
zao za kupigia kura zinaonyesha kutokuwa niza wakazi wa jimbo la Kalenga.
“Kweli nimeweka pingamizi kwa mgombea mwenzagu wa CCM Godfrey
Mgimwa, na niliweka hilo baada ya kusoma fomu yake iliyobandikwa kwenye ukuta
ambapo mgombea Mgimwa alionyesha kuwa na mapungufu mbalimbali likiwemo la kutokuwa raia wa Tanzania, pili katika fomu yake aliyodhaminiwa
wadhamini wake hawakutoka Kalenga, na hili tuna ushahidi nalo, kwani kuna shahada
za kupigia kura zinaonyesha baadhi ya wadhamini wametoka Songea, Njombe na Iringa vijijini
na siyo jimbo la Kalenga- Lakini lingine ni juu ya kiasi cha fedha za kuendeshea kampeni ambacho kila mgombea alipaswa kuweka bayana ili kuujulisha Umma kuwa ni kiwango gani kitatumika katika kuendeshea kampeni na hili nila sheria za gharama za uchaguzi,
lakini Mgimwa hakujaza kiasi chake cha fedha katika fomu hiyo, hilo nalo limo ndani ya pingamizi,” Alisema Tendega.
Aidha Tendega amesema hata tarehe ya uteuzi mgombea wa CCM
amejaza kuwa ni tarehe 16 mwezi wa tatu mwaka 2014 badala ya tarehe 18 mwezi wa
pili jambo linaloonyesha CCM bado wanasubiri uteuzi utakaofanyika tarehe 18
mwezi wa tatu na kuwa mgombea aliyopo sasa hafai kushiriki katika kampeni zozote kwa sasa.
Pia Tendega amesema pingamizi lingine ni uwepo wa sahihi tofauti
zilizopo katika fomu za udhamini na zile zilizo katika vitamburisho vya kupigia
kura, jambo linaloonyesha mgombea wa CCM kuwa na mapungufu ya vigezo vya kushiriki kampeni na uchaguzi huo.
Mratibu wa CHADEMA kanda ya kusini Frenk Mwaisumbe amesema
CHADEMA inafuatilia kwa makini kila kitu na kuwa ipo haja kwa tume ya Taifa ya
uchaguzi kutenda haki kwa vyama vyote pasipo kubagua kama kuna uvunjifu wa sheria za uchaguzi.
Hata hivyo msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo la Kalenga Bi. Pudensiana
Kisaka amesema amepokea pingamizi hilo siku ya tarehe 19 majira ya saa
tisa jioni, kutoka kwa mgombea wa CHADEMA
Grace Tendega dhidi ya Godfrey Mgimwa na kuwa kazi yake kama msimamizi
ni kumuandikia barua mgombea aliyewekewa pingamizi hilo huku barua hiyo
ikiambatana na Pingamizi.
Kisaka amesema mgombea aliyewekewa Pingamizi baada ya kupata
barua iliyoambatana na pingamizi kutoka kwa mgombea wa CHADEMA, amejibu shutuma zinazomkabiri, na kuwa upande uliotoa Pingamizi (CHADEMA)
unapaswa kupeleka vielelezo katika ofisi yake ya msimamizi mkuu wa uchaguzi haraka iwezekanavyo.
“Mimi nikipokea pingamizi ninapaswa kumuandikia barua
na kumpatia mgombea aliyewekewa pingamizi hilo huku barua hiyo nikiambatanisha na pingamizi
alilowekewa, na katika kifungu cha 40
cha sheria ya uchaguzi kifungu kidogo cha 4 ”a” kinaruhusu kutoa uamuzi kwa
pande zote mbili na kama upande mmoja haujaridhika unaweza kukata rufaa,”
alisema Kisaka.
Wakati hayo yote yakiendelea kampeni za uchaguzi kwa mujibu
wa tume ya Taifa ya Uchaguzi tayari zimeanza tangu tarehe 19 mwezi huu wa pili licha ya kuwa kila chama kinataraji kuzindua
rasmi kampeni zake kwa kuwashirikisha viongozi wa vyama vyao Kitaifa.
MWISHO
No comments:
Post a Comment