Wednesday, March 21, 2012

SERENGETI YASAIDIA MILIONI 300 KATIKA HUDUMA YA MAJI


KAMPUNI ya Serengeti Brewieries inayozalisha vinywaji  mbalimbali kama Tusker, Uhuru, The kick,  Seringeti  nk. imetenga zaidi ya shilingi  Milioni 300  ili kuboresha huduma ya maji
katika mkoa wa Iringa.

Akizungumzia mpango huo mbele ya naibu waziri wa maji Gerson Lwenge,wakati wa uzinduzi wa mradi huo wa kuvuna maji ya mvua katika Hospitali ya Manispaa ya Iringa, ofisa uhusiano wa kampuni ya Serengeti Breweries Bi. Tedy Mapunda,  amesema kampuni imemeamua kuwekeza katika huduma ya maji kwa jamii.

Tedy amesema kati ya fedha hizo, shilingi milioni 200 mwaka huu  wamewekeza katika miradi salama ya maji, ikiwa pamoja na uvunaji wa  maji ya mvua katika Hospitali mpya ya Manispaa ya Iringa.

Amesema wameanzisha mpango wa kutoa elimu kwa jamii, ili kuvilinda  vyanzo vya maji na miundombinu yake, ikiwa pamoja na kuweka matenki ya  lita elfu 60 kwa ajili ya kuvuna maji katika Hospitali hiyo.

Aidha amesema lengo la mpango huo ni kurejesha huduma kwa jamii,  kutokana na kampuni hiyo ya Serengeti kutumia huduma ya maji kwa  kiwango kikubwa katika uzalishaji wa bidhaa zake.

Naye Naibu waziri Lwenge amezindua ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji  ya mvua, ambalo litagharimu zaidi ya shilingi Milioni 50  zinazotolewa  na Kampuni ya Serengeti, huku Milioni 150 zitapelekwa katika Hospitali
ya Seketule Mwanza pamoja na Hospitali ya Mawenzi Kilimanjaro na Dar  es salaam katika Hospitalia ya Temeke.

Ofisa uhusiano wa kampuni ya Serengeti Bi. Teddy Mapunda akieleza malengo ya kampuni kujikita katika masuala ya kuchangia  huduma ya maji kwa wananchi,  akiwa katika Hospitali ya Manispaa ya Iringa, Uzinduzi uliofanywa na Naibu waziri wa maji, Mh. Geryson Lwenge.
 

No comments:

Post a Comment