Thursday, May 10, 2012




MASIKINI WANAFUNZI HAWA!!

  wanafunzi hawa wanachota maji katika mfereji wa maji ya umwagiliaji Mbarali.

WANAFUNZI  wa shule ya msingi Rujewa iliyopo katika Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya wakitumia mbinu ya kushikana mikono ili kuchota maji, mbinu ambayo ni hatari  zaidi kwa usalama wa maisha yao, kwani mmoja atakapoachia mkono wa mwenzie wanaweza wakatumbukia.

Wilaya ya Mbarali inakabiliwa na shida ya maji kutokana na hifadhi ya Mpanga Kipengele kuzuia Halmashauri kutoendeleza mpango wa ujenzi wa huduma ya maji katika eneo hilo ambalo ni poli la akiba lililopo katika Mkoa wa Njombe na Mbeya katika Wilaya ya Mbarali.

No comments:

Post a Comment