Mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo
cha televisheni cha Channel Ten Daud Mwangosi leo amefikishwa
tena katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi ya Wilaya kujibu shitaka
lilalomkabili.Huku akiwa chini ya ulinzi mkali wa askari.
Akisomewa shitaka lake na mwendesha mashtaka wa serikali Mkuu
Lilian Ngilangwa , alisema mtuhumiwa huyo ambaye ni askari mwenye namba G2573
Pasificus Cleophace Simoni (23) mkazi wa FFU Iringa, anakabiliwa na shitaka la
mauaji ya makusudi.
Alisema mtuhumiwa huyo mnamo 02 Septemba mwaka huu katika kijiji
cha Nyololo Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa alimuua Daudi Mwangosi kwa
makusudi kinyume na kifungu cha sheria namba 148 kifungu kidogo 5 (a) i cha
makosa ya jinai.
Hakimu Mkuu Mwandamizi wa mahakama ya Wilaya Dyness Lyimo alisema
mtuhumumiwa hatatakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kuendesha
kesi za mauaji.
Kwa mujibu wa kesi za jinai, sheria kifungu 196 kanuni ya adhabu
sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002, kinakataza mtuhumiwa wa mauaji ya
kukusudia kupewa dhamana.
Mtuhumiwa amerudishwa mahabusu kutokana na kesi yake kukosa
dhamana kisheria na kesi hiyo imeahirishwa hadi 10 Oktoba mwaka huu
itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Hata hivyo askari wengi waliompeleka mtuhumiwa huyo wakiwa
wamevaa nguo za kiraia walihakikisha kuwa mtuhumiwa huyo hapigwi picha jamba
ambalo limewaletea ugumu kwa mara ya pili waandishi wa habari waliokuwapo katika
mhakama hiyo kwani walisukumwa na kuzuia kumpiga picha mtuhumiwa huyo, huku
mtuhumiwa akiwa amejifunika kichwa na kuvaa miwani mieusi kuhakikisha kuwa sura
yake haionekani.
Lakini jambo la kushangaza mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani
hapo kwa gari binafsi la kifahari lenye namba za usajili DFP 2175 Toyota Land
cruiser tofauti na watuhumiwa wengine ambao walifikishwa mahakamani hapo kwa
gari la polisi(Karandinga), gari hiyo ikiwa tofauti na ile ya awali ambayo
ilikuwa namba T
320 ARC ambapo pia alivalia kodi kubwa jeusi refu huku kichwani akiwa
amejifunika kwa kitambaa kwa ulinzi mkali wa maofisa wa jeshi la
polisi.
polisi.
Ambapo mwendesha
mashtaka mkuu wa serikali, mkoa wa Iringa Michael Luena alisema kesi hiyo namba 01.RM ya
mauaji kifungu namba 196, ipo chini ya kanuni za adhabu sura ya 16
marejeo ya mwaka 2012.
Luena alisema mtuhumiwa huyo mwenye namba G. 2573 Pasificus Creophace Simion 23, kabila Muhaya na mkazi wa FFU anatuhumiwa kwa kosa la mauaji (Mada) ambapo alitenda kosa hilo katika kijiji cha
Nyololo, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, siku ya tarehe 2 ya mwezi wa tisa (Septemba) 2012, kwa kumuua Daud Mwangosi.
Mtuhumiwa pia hakutakiwa kujibu lolote, kutokana na mahakma hiyo kutokuwa na uwezo wa kuendesha kesi za mauaji na hivyo hakimu Dyness kuamuru mtuhumiwa apelekwe magereza hadi tena kesi hiyo itakapotajwa tena tarehe 26 mwezi wa tisa, kutokana na kesi yake kutokuwa na dhamana.
Ambapo msaada wa wanasheria mahakamani hapo, walisema kesi hiyo ya mada ina maana ya kuua kwa kukusudia na uendeshaji wa kesi hizo una hatua nyingi hadi ushahidi ukamilike , ambapo mtuhumiwa hatakuwa na uwezo wa kujibu chochote katika ngazi ya mahakama hiyo.
“Kesi hii ya mada ina mana aliua kwa kukusudia, ndiyo maana dhamana yake imezuiliwa, lakini ingekuwa ya kuua bila kukusiudia dhamana yake ingekuwa wazi,” Alieleza mmoja wa wanasheria wa mahakama hiyo.
Alisema hatua hiyo inatokna na kifungu cha 148 kifungu cha 5 - "a" 1 (Roman One) ambacho kinazuia dhamana kwa baadhi ya makosa ikiwemo kosa la mauaji ya kukusudia.
Walisema kifungu hicho kinamnyima dhamana mtuhumiwa na anatakiwa kwenda Magereza ambapo sasa ni mahabusu hadi kesi yake upelelezi wake utakapokamilika.
MWISHO
Luena alisema mtuhumiwa huyo mwenye namba G. 2573 Pasificus Creophace Simion 23, kabila Muhaya na mkazi wa FFU anatuhumiwa kwa kosa la mauaji (Mada) ambapo alitenda kosa hilo katika kijiji cha
Nyololo, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, siku ya tarehe 2 ya mwezi wa tisa (Septemba) 2012, kwa kumuua Daud Mwangosi.
Mtuhumiwa pia hakutakiwa kujibu lolote, kutokana na mahakma hiyo kutokuwa na uwezo wa kuendesha kesi za mauaji na hivyo hakimu Dyness kuamuru mtuhumiwa apelekwe magereza hadi tena kesi hiyo itakapotajwa tena tarehe 26 mwezi wa tisa, kutokana na kesi yake kutokuwa na dhamana.
Ambapo msaada wa wanasheria mahakamani hapo, walisema kesi hiyo ya mada ina maana ya kuua kwa kukusudia na uendeshaji wa kesi hizo una hatua nyingi hadi ushahidi ukamilike , ambapo mtuhumiwa hatakuwa na uwezo wa kujibu chochote katika ngazi ya mahakama hiyo.
“Kesi hii ya mada ina mana aliua kwa kukusudia, ndiyo maana dhamana yake imezuiliwa, lakini ingekuwa ya kuua bila kukusiudia dhamana yake ingekuwa wazi,” Alieleza mmoja wa wanasheria wa mahakama hiyo.
Alisema hatua hiyo inatokna na kifungu cha 148 kifungu cha 5 - "a" 1 (Roman One) ambacho kinazuia dhamana kwa baadhi ya makosa ikiwemo kosa la mauaji ya kukusudia.
Walisema kifungu hicho kinamnyima dhamana mtuhumiwa na anatakiwa kwenda Magereza ambapo sasa ni mahabusu hadi kesi yake upelelezi wake utakapokamilika.
MWISHO
No comments:
Post a Comment