Baadhi ya wateja wa Benki ya wananchi wa Mufindi- MUCOBA wakipatiwa huduma za kifedha.
Ben Mahenge meneja mauzo wa benki ya Wananchi wa Mufindi- MUCOBA akiwa nje ya jengo la benki hiyo akitoa maelekezo.
Meneja mauzo wa Benki ya wananchi wa Mufindi - MUCOBA Bw. Ben Mahenge akitoa ufafanuzi wa malengo ya benki hiyo.
Meneja mauzo wa Benki ya wananchi wa Mufindi - MUCOBA Bw. Ben Mahenge akiwa na Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa.
BENKI ya wananchi wa Wilaya ya Mufindi –
MUCOBA, imetoa mikopo ya shilingi Bilioni 1.3 kwa zaidi ya wakulima 1000 wa Wilaya ya Kilolo, kwa lengo la
kuinua shughuli hizo za kilimo ili kuwawezesha wakulima kuendesha kilimo bora
nacha kisasa.
Akizungumzia mpango huo wa mikopo
kwa kundi hilo la wakulima, meneja mauzo wa benki ya wananchi Mufindi- MUCOBA, Ben Mahenge alisema mpango huo umelenga kutanua wigo wa utoaji wa huduma za
benki hiyo ya MUCOBA-kutoka Wilaya ya Mufindi hadi kuzifikia Wilaya zote za
mkoa mzima wa Iringa.
Mahenge alisema utoaji wa huduma za
kifedha MUCOBA inakabiliwa na changamoto kubwa ya umbali katika kuwafikia
wananchi waishio vijijini, huku baadhi ya wateja wasio waaminifu wakishindwa kurejesha
mikopo kwa wakati.
Aidha alisema kukosekana kwa elimu kwa
baadhi ya wananchi hususani waishio vijijini - ni moja ya sababu inayoikabili jamii, huku baadhi yao wakishindwa kuelekeza
fedha za mikopo katika malengo yaliyokusudiwa hatua inayosababaisha MUCOBA kuwa
na madeni chechefu ya zaidi ya shilingi Milioni 600.
“Kuna baadhi ya maeneo tunalazimika
kutembea umbali wa km 150 kuwafuata wateja, lakini unakuta kuna baadhi ya
wateja ambao sio waaminifu wanashindwa kurejesha mikopo yao, hii inatokana na
kukosekana kwa elimu ya mikopo kwa wananchi,” Alisema Mahenge.
Alisema ipo haja kwa taasisi za
kifedha kutoa elimu hiyo kwa wananchi ili kutambua umuhimu wa kuhifadhi fedha benki,
ikiwa pamoja na kuwa na uelewa juu ya mikopo ili kuepuka mali zao kubinafsishwa
baada ya kushindwa kurejesha mikopo.
Hata hivyo Mahenge alisema benki
hiyo imekusudia kuwafikia wananchi wa mkoa mzima wa Iringa, na baada ya
kuwafikia wananchi wa Wilaya aya Kilolo wameanza kufanya harakati za kufikisha
huduma hiyo Manispaa ya Iringa.
MWISHO
No comments:
Post a Comment