Kibao cha shule y msingi Ndulamo
Na Edwin Moshi, Makete
Shule
ya msingi Ndulamo iliyopo kijiji cha Ndulamo wilayani Makete mkoani Njombe, ipo
hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na kuhara kutokana
na kukosekana kwa huduma ya maji.
Akizungumza
na mtandao huu ofisini kwake mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw. Godigodi Bosco
Malangalila amesema tatizo hilo nila muda mrefu na hivyo kutishia usalama wa
walimu na wanafunzi.
Malangalila
amesema tatizo hilo linahatarisha afya za wanafunzi wake kwani pamoja na
ukosefu huo wa maji wakati mwingine shule hulazimika kuvunja vipindi na
kuwaagiza wanafunzi kwenda kuchota maji kwenye mito ama visima ambayo si safi wala
salama na kulazimika kuyatumia.
“Ndugu
mwandishi inasikitisha kwa kweli, hapa shuleni huwa tunatoa uji kwa wanafunzi
lakini maji hata ya kuosha vyombo hakuna, ya kutumia vyooni nayo hakuna na vyoo
vya shule ni vile vya kutumia maji, lakini wanafunzi huenda kujisaidia hivyo
hivyo bila maji” alisema Mwalimu Malangalila,” amesema.
Aidha
amesema mara nyingi vyoo vya shule huziba na kulazimika waalimu wenyewe
kuvizibua na wakati wengine kuwaita wazazi kuja kuzibua vyoo hivyo lakini hivi
sasa wazazi wengi hugoma kuja kufanya shughuli hiyo kwa madai kuwa wao
wanachanga fedha za maji kijijini hivyo ni jukumu la vyombo husika kufikisha
maji shuleni hapo ili kuinusuru shule hiyo.
Akiongezea
Malingalila amesema “Tangu nimefika hapa shuleni kama mwalimu mkuu mwezi Julai
2012, nimeshafunga shule kwa tatizo hili hili, kwa kuwa tunazidiwa,” alisema
Katika
hatua nyingine mwalimu huyo amesema tatizo hilo la ukosefu wa maji pia
limeathiri ujenzi wa nyumba ya mwalimu shuleni hapo ambapo ujenzi huo ulikuwa
ukamilike Oktoba mwaka jana lakini hadi hivi sasa nyumba hiyo imefikia sehemu
ya linta, kwa tatizo kubwa ni ukosefu wa maji
Kwa
upande wake Tamali Cyprian Sanga mwanafunzi anayesoma darasa la saba shuleni
hapo ambaye pia ni dada mkuu wa shule hiyo amesema tatizo hilo linawathiri kwa
kiasi kikubwa wao wanafunzi, kwani huwalazimu kuosha vyombo vya chakula kwa
kutumia maji machafu, huku wakikosa baadhi ya vipindi kwa kwenda kuchota maji mtoni.
“Visima
vipo mbali na shule pia vyoo tunavyotumika kwa hivi sasa ni vichafu na hakuna
maji ya kuvifanyia usafi na tunalazimika kuvitumia hivyo hivyo,” Amesema.
Naye
kaka mkuu wa shule hiyo Alexanda Marko amesema wakati mwingine kutokana na
uchafu uliokithiri kwenye vyoo hivyo hulazimika kurudi nyumbani kujisaidia huku wengine wakijisaidia kwenye
msitu wa shule hiyo ambao uko jirani na kuwataka wahusika kulishughulikia
ipasavyo tatizo hilo.
Shule ya
Msingi Ndulamo ina jumla ya wanafunzi 633 ambao wanategemea maji ili kuendesha
shughuli mbalimbali katika shule hiyo.
MWISHO
No comments:
Post a Comment