Baadhi ya wanachuo wanaotoka katika jamii ya wafugaji, wanaosoma katika vyuo vikuu mkoani Iringa, wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza mkutano wa utoaji wa tamko juu ya ardhi ya Loliondo.
Bw. Solomon Lekui, akisikiliza maoni ya wanaumoja baada ya kusoma tamko la wanachuo wanaotoka katika jamii ya wafugaji.
Bi. Nesale Rorian na wenzake wakisikiliza maoni ya wachangiaji wa tamko hilo.
Bw. Solomon Lekui, akisikiliza maoni ya wanaumoja baada ya kusoma tamko la wanachuo wanaotoka katika jamii ya wafugaji.
Bi. Nesale Rorian na wenzake wakisikiliza maoni ya wachangiaji wa tamko hilo.
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mkutano wa kutoa tamko.
HATIMAYE wanafunzi wa jamii ya
wafugaji, wanaosoma katika vyuo vikuu mkoani Iringa, wameungana na kutoa tamko
juu ya mgogolo wa Loliondo mkoani Arusha, huku wakimtaka waziri mwenye dhamana
ya maliasiri na Utalii, Barozi Khamis Kagasheki kurejea upya namna ya kufanya utatuzi wa mgogolo huo.
Tamko hilo limetolewa na umoja wa
wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Iringa wanaotoka katika jamii ya wafugaji, mkutano
uliofanyika katika ukumbi wa Hotel ya Country Side iliyopo katika eneo la
Tumaini mjini Iringa.
Akisoma tamko la wanachuo hao
Solomon Lekui ambaye ni mjumbe wa umoja wa jamii ya wafugaji wanaosoma vyuo
vikuu mkoani Iringa, amesema kamwe hawapo tayari kushuhudia wazazi wao
wakipokonywa ardhi ambayo ni mali yao halali.
Lekui alisema wanapinga vikali amri
ya waziri Barozi Khamis Kagasheki aliyoitoa tarehe 26 mwezi wa 3 mwaka huu
akiwataka kuhamisha katika makazi yao wananchi wa Loliondo wanaoishi katika eneo
linalodaiwa na serikali kuwa ni poli tengefu (Loliondo Game Controlled Area)
ambalo lina ukubwa wa kilomita za mrab
elfu 4.
Lekui alisema eneo hilo mabalo linamilikiwa
na vijiji vya Ololosokwan, Soitsambu, Oloipiri, Oloirien, Maloni, Arash,
Malambo na Piyaya vijiji vilivyopo ndani ya Loliondo ni mali halali ya wananchi
hao, na si vyema serikali kuchukua uamuzi wa kuwaondoa wananchi hao.
Emmanuel Ole Kileli mwanafunzi
kutoka chuo kikuu cha Tumaini alisema imekuwa kama desturi kwa wafugaji
kulalamika juu ya mambo mbalimbali yanayohusiana na unyang’anyi wa ardhi yao
inayoambatana na uhamishaji kwa kutumia nguvu na upotevu mkubwa wa mali na
maisha yao.
Ole Kileli lisema Serikali imekuwa mstari
wa mbele katika kutekeleza maamuzi magumu kwa wafugaji nchini, kwa madai kuwa
wafugaji wanakiuka sheria kwa kuvamia maeneo mbalimbali yasiyo ya ufugaji hasa
maeneo ya hifadhi naya kilimo, na kuwa hatua hiyo ni kutokana na kukosekana kwa
sera ya ufugaji asili (Pastoralism
Policy) ambayo ingehusika kuratibu na kuthamini shughuli mbalimbali za
ufugajiasili na mazao yake kwa ujumla.
Saikon Justin mwenyekiti wa jumuiya
ya wanafunzi wanaotoka katika jamii ya
wafugaji alisema serikali inapaswa kutafakari vizuri suala la wafugaji kitaifa,
na kutafuta suluhu ya kudumu kwani imepelekea wafugaji kote nchini kuiona
serikali ya Tanzania kama adui mkubwa kupitia upotevu wa mali na haki zao za
msingi kama watanzania siku hadi siku.
“Serikali na wadau kote nchini
waache kubeza ufugaji asili kwa
madai ya kuwa hauna tija na huchangia kiwango kidogo cha pato la Taifa, kwani ukweli
ni kuwa tafiti nyingi zinaonyesha ufugaji
asili una tija na unaliongezea taifa kipato hasa katika ngazi ya
Halmashauri ambazo zina mifugo mingi
kwani imekuwa ikipata ushuru kupitia sekta hiyo ya Mifugo,” Alisema Saikon.
Samaito Olekopitoo alisema sekta ya
Ufugaji inachangia pato la Taifa kwa kiwango kikubwa kwani inatoa ajira nyingi kuanzia
ngazi ya kijiji hadi Taifa, kuanzia kwa wafugaji wenyewe, wafanyabiashara wa
mifugo na mazao yatokanayo na mifugo, wakiwemo wamiliki wa Bucha, Maeneo ya
nyama choma, Hotel, Vibanda vya Chips na wafanyakazi wao kwa ujumla, kwa hiyo
sekta ya mifugo ina tija na maslahi kwa
Taifa.
Aidha waliiomba serikali iundwe
Tume maalumu ya kukusanya maoni ya wafugaji kote nchini ili kutafuta namna ya kutatua
kikamilifu mgogolo huu, kwa kutumia ushirikishwaji wa matatizo ya wafugaji kote
nchini.
Kwa madai kuwa kuna haja ya
kutafuta suluhu ya kudumu kwa kuunda sera ya Ufugaji asili ili kuondo ufugaji ndani ya sekta ya kilimo, kwa
madai kuwa tafiti mbalimbali zinazoonyesha suala la ufugaji kwenda sambamba na
kilimo siyo sahihi hata kidogo.
Nesale Rorian alisema wafugaji na
wakulima hawawezi kutekeleza shughuli zao pamoja, na inaonekana kupitia migogolo mingi ambayo
imekuwa ikitokea baina ya wafugaji na wakulima, huku vipaumbele kwenye suala la
kilimo, -ufugaji vikiwa haupewi fulsa ya kutosha kama ilivyo kwa kilimo, na
kaulimbiu ya KILIMO KWANZA, kwani
hapo suala la Ufugaji halikupewa kipaumbele vya kutosha.
Pamoja na hayo wanachuo hao waliitaka
serikali iangalie upya maeneo ya wafugaji kupewa wawekezaji pasipo wafugaji
wenyewe kushirikishwa na hivyo kuondoa dhana kuwa maeneo ya wafugaji ni maeneo
ya wazi na hayana mmiliki.
“Hii ni athari kubwa kwa wafugaji
hasa katika ngazi za Halmashauri ambazo wafugaji ni wachache katika hatua ya
maamuzi, kwani bajeti zinazopitishwa kwa ajili ya masuala ya ufugaji ni ndogo,
huku wataalamu wa mifugo wakishughulika
na masuala ya kilimo,” Walisema.
Keko Olekijepe alisema ufugaji asili ni mfumo wa maisha kama
ilivyo mifumo mingine yoyote, na hivyo ni vyema na haki mfumo huu wa Ufugaji
ukaheshimiwa na kupewa fulsa kama mifumo mingine katika nchi yetu tukufu ya
Tanzania, na kuwa ufugaji asili ukiratibiwa vizuri hauharibu mazingira, tofauti
na kilimo ambacho kinachangia moja kwa moja kuharibu uoto wa asili kwa ukataji
miti na kuharibu Ikolojia.
MWISHO
No comments:
Post a Comment