Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, Gerlad Guninita (wapili kushoto) akitoa amri ya kukamatwa viongozi katika uwanja wa mkutano wa kijiji cha Mlafu. (kulia ni kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya hiyo.
Kituo cha Polisi cha Mbigili ambacho viongozi hao wameshikiliwa kwa kukaidi amri ya kuitisha mkutano wa utatuzi wa mgogolo wa wananchi.
Uwanja wa mkutano ukiwa na msafara wa mkuu wa Wilaya pekee.
KATIKA
hali isiyo ya kawada, viongozi wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, wamemchezea
mchezo mchafu mkuu wa Wilaya hiyo ya Kilolo Gerlad Guninita, kwa kumuita katika
mkutano usio na wananchi, ambao ulilenga utatuazi wa mgogolo wa ardhi.
Tukio
hilo la aina yake limetokea baada ya mkuu huyo kufunga safari ya kuitika wito
huo, ambao ulilenga utatuzi wa mgogolo wa ardhi ambayo imechukuliwa kwa kiasi
kikubwa na mtu mmoja jambo ambalo ni uvunjwaji wa sheria za ardhi, huku akikuta katika uwanja wa mkutano hakuna wananchi jambo lililompandisha hasira mkuu huyo.
MKUU
huyo alifika katika eneo la mkutano majira ya saa sita kasoro na kukaa kwa zaidi ya saa moja bila mafanikio ya kuwapata wananchji, jambo lililobainisha mapungufu katika utendaji wa kazi wa viongozi hao na mkuu huyo kutoa amri kwa askari polisi walioambatana na msafara huo kuwakamata viongozi hao waliosababisha hasara kubwa kwa Halmashauri hiyo.
Guninita
alijikuta katika mkutano huo akiwa yeye, kamati ya ulinzi na usalama, wataalamu
wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo pamoja na wanahabari ambao walikuwa
wameambatana nae katika msafara huo.
Mkuu
huyo wa wilaya ya kilolo alisema hakuna haja ya kuwachekea viongozi wsa aina
hiyo, ambao hawatilii maanani vilio vya wananchi wao, kwa kupuuzia muafaka wa
mgogolo huo unaowasumbua wananchi.
“Sioni
sababu ya kuwachekea watu wa aina hii, hawa ndiyo wanachangia kudhorotesha maendeleo, OCD hakikisha unaondoka na hawa
viongozi, ofisa tarafa wa tarafa ya Mazombe na huyu kaimu mtendaji wa Kata hii
ya Mlafu, siwezi nikafunga safari ndefu kutoka kilolo na msafara mzima halafu nafika hapa
hakuna wananchi, kama kulikuwa na tatizo kwa nini msingenijulisha kwa simu ili nisipoteze muda wangu nawa wataalamu wangu hawa, hawa wakakae Rock up hadi kesho ili liwe fundisho kwa viongozi wa
aina hii hapa Kilolo,” Alisema Guninita.
Alisema
viongozi hao kupitia mikutano yao ya awali walimuomba afike kijijini hapo ili
kufanya mazungumzo na wananchi wa kijiji hicho juu ya mgogolo huo wa ardhi, na
walimtaka tarehe 30 mwezi uliopita naye aliomba udhuru kwakuwa alikuwa na kikao
cha utoaji wa taarifa ya utekerezaji wa shughuli za maendeleo, wakampangia mkuu
huyo wa Wilaya afike tarehe 7 ya mwezi huu Mei
kuzungumza na wananchi na hatimaye kuikuta hali hiyo.
Seljo
Nyauhele, mjumbe wa serikali ya kijiji cha Mlafu na Festo Kakoko mwenyekiti wa
akitongoji cha Masukanzi walisema wanaungana na hatua ya mkuu huyo wa Wilaya,
kwani licha ya kuwepo kwa dharula ya msiba viongozi hao walipaswa kuandaa
mazingira ya mkutano ili wananchi wapate muafaka wa tatizo lao linalowakabili
kwa muda mrefu.
Naye
Gaitan Mwagala, diwani wa Kata aya Mlafu alisema siku ya nyuma walikuwa
walijadili na kupanga masuala mbalimbali ya mkutano huo, na aameshangazwa kukuta uwanja wa mkutano ukiwa hauna watu.
“Unajua
kuna haja ya kupeana adhabu pale tunapofanya ndivyo sivyo, jana tulikuwa na
kikao cha ODC, tukakubaliana kutengeneza mazingira ya mkutano, lakini
ninashangaa kuona hali hii, watu wengine wafundishike kwa namna hiyo,”
Alisema Mwagala.
Waliokamatwa
na kuswekwa lumande ni pamoja ofisa tarafa wa tarafa ya Mazombe Silvanus
King’ung’e na Kaimu mtendaji wa Kata hiyo ya Mlafu Thomas Nyabangi ambapo walifungiwa katika Lumande ya kituo cha
Polisi cha Mbigili.
Hata
hivyo mkuu huyo wa Wilaya Guninita amesema hatua hiyo ni fundisho kwa viongozi
wengine ambao wamekuwa wakipuuzia maagizo yenye maslahi kwa wananchi, huku
baadhi ya wananchi na viongozi wa kijiji hicho wakiunga mkono hatua ya mkuu
huyo.
Moja ya hasara zilizotokana na uzembe wa viongozi hao, ni pamoja na Halmashauri kujingia hasara ya matumizi yasiyo ya halali ya mafuta ya magari ambayo yaliwabeba wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, gari la kamati ya ulinzi na usalama, gari la wanahabari pamoja na gari la mkuu wa Wilaya mwenyewe, jambo ambalo litachangia matumizi yasiyo ya halali ya fedha za wananchi (Walipakodi).
MWISHO
No comments:
Post a Comment