Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Mlafu kilichopo tarafa ya Mazombe Wilaya ya Kilolo wakimsikiliza mkuu wa Wilaya hiyo Gerlad Guninita, alipofika kutatua mgogolo wa ardhi unaowakabiri wananchi hao.
"Tupo makini sana mkuu, ni kma wanasema hivyo wananchi wa Mlafu.
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Gerlad Guninita akizungumza katika mkutano huo wa hadhara katika kijiji cha Mlafu.
Diwani wa Kata ya Mlafu akikabidhi zawadi ya Mkungu wa Ndizi kwa DC-Guninita.
Mwananchi wa kijiji cha Mlafu akikabidhi zawadi.
Mwananchi (Kilungu) akikabidhi zawadi kama ishara ya furaha yake baada ya mkuu huyo kumaliza mgogolo unaowasumbua kwa zaidi ya mika 5.
Mjumbe wa serikali ya kijiji akikabidhi naye zawadi.
Diwani wa Kata ya Mlafu akikabidhi zawadi ya Mkungu wa Ndizi kwa DC-Guninita.
Mwananchi wa kijiji cha Mlafu akikabidhi zawadi.
Mwananchi (Kilungu) akikabidhi zawadi kama ishara ya furaha yake baada ya mkuu huyo kumaliza mgogolo unaowasumbua kwa zaidi ya mika 5.
Mjumbe wa serikali ya kijiji akikabidhi naye zawadi.
Mmiliki wa eneo hilo ambalo kisheria aliuziwa ndivyo sivyo (mwenye koti la Kijani) Kiyenge akitoa maneno ya kukabidhi ardhi hiyo mbele ya mkuu wa Wilaya.
Mazungumzo katika shamba la Mahindi zaidi ya ekari 5, shamba ambalo limenusulika kuvunwa na wananchi, na hivyo kukemewa na mkuu wa Wilaya kutofanya uharibifu huo.
Ofisa Wilayani Kilolo, akiambatana na msafara, ambao nyumba yake ni mwekezaji wa ardhi Kiyenge akiwa na mpambe wake Kilungu, baada ya kukabidhi ardhi mikononi mwa serikali ya kijiji cha Mlafu.
HATIMAYE mkuu wa Wilaya ya Kilolo
mkoani Iringa Gerlad Guninita ambaye siku za hivi karibuni aliwaweka Lumande
watumishi wa Halmashauri hiyo ya Kilolo, amemaliza mgogolo uliokuwa unawakabili
wananchi wa kijiji cha Mlafu kwa zaidi ya miaka mitano.
Lakini cha kushangaza ni pale mkuu
huyo Guninita alipopokewa kwa shangwe, Nderemo na Vifijo baada ya maofisa hao
kuandaa vilivyo mapokezi ya mkuu huyo, zikiwemo ngoma za jadi, Vyakula Zawadi mbalimbali pamoja na
mapokezi ya aina yake.
Uwepo wa idadi kubwa ya wananchi
waliofika katika mkutano huo pia uliwashangaza hata viongozi na wananchi wenyewe
na kudai kuwa hali hiyo haijawahi kutokea na nihistoria katika kijiji hicho.
Guninita katika mkutano huo pia
aliandaliwa Nyimbo na mashairi yenye jumbe mbalimbali ikiwa ni zawadi na furaha
ya ujio wake wa awamu nyingine, na kubwa likiwa ni wananchi kufurahia hatua ya kiongozi
huo wa Wilaya kukomalia utatuzi wa mgogolo huo.
Aidha Guninita alifanikiwa kumaliza mgogolo huo ambao kwa mujibu wa mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha
Mlafu, wametumia gharama kubwa katika kufuatilia mgogolo huo Halmashauri ya Wilaya hiyo pasipo na mafanikio kwa zaidi ya miaka mitano.
Pia mkuu huyo alisema kuna kila
haja wataalamu wakatoa elimu kwa wananchi juu ya ardhi ili kutambua sheria
zinazowataka katika utoaji wa ardhi za kijiji, kwani serikali ya kijiji haina
uwezo wa kutoa ardhi zaidi ya ekari 50 kwa mtu mmoja.
Akitaka ufafanuzi zaidi juu ya
ardhi hiyo iliyorudishwa mikononi mwao, mwananchi Elia Muhema alitaka kufahamu
juu ya mazao yaliyokuwepo katika shamba hilo, ambapo mkuu huyo aliwataka
wananchi wamuache mwekezaji huyo aondoe mazao yake (Mahindi) ili kuendeleza upendo na mshikamano baina yao.
“Kama kuna mazao jamani hayo mazao
ni mali yake, mumuache avune Mahindi yake, nadhani hadi mwezi wa saba atakuwa
tayari ameyaondoa,” Alisema Guninita.
Mzee Elias Msola alimpongeza mkuu
huyo kwa jitiohada zake za kumaliza mgogolo huo, huku mwekezaji Kiyenge naye
akishukuru kwa hatua ya kiongozi huo, ambapo msafara mzima na baadhi ya
viongozi wa serikali ya kijiji hicho cha Mlafu ulifunga safari hadi katika eneo
hilo lenye mgogolo.
Kiyenge alisema awali alihofia
mazao yake kutaifishwa na wananchi hao, jambo lililomkosesha amani, na kuwa
uamuzi wa mkuu huyo umezingatia haki, na kuwa ardhi hiyo ameirudisha kwa amani
na atafuata taratibu za kisheria ili kupata kiwango sahihi kinachotakiwa.
Hata hivyo furaha ya wananchi hao
na viongozi wa serikali ya kijiji haikuishia hapo, kwani maandalizi makubwa ya
chakula yalifanyika, huku wale viongozi waliowekwa Lumande katika kituo cha
Polisi cha Mbigili kilichopo tarafa ya Mazombe wakionyesha furaha tofauti na
hisia za wengi walivyodhani.
No comments:
Post a Comment