Tuesday, October 9, 2012

TCCIA YALIA NA LUMBESA INAVYOWAMALIZA WAKULIMA


Mkamu mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Iringa, Bw. Henry Mangenya akifuatilia jambo katika moja ya mafunzo ya wafanyabiashara katika Kata ya Matamba wilaya ya Makete, mkoa mpya wa Njombe (Iringa)


Mshauri mwezeshaji wa TCCIA mkoa wa Iringa Bw. Dustun Mpangala akitoa mafunzo kwa wafanyabiashara, hiyo ikiwa ni moja ya kufikisha elimu juu ya madhara ya Lumbesa. 


Bw. Dustun Mpangala akitoa mafunzo kwa wafanyabiashara, 

Mkufunzi Bw. Dustun Mpangala akitoa mafunzo kwa wafanyabiashara, 

Mmoja wa wanufaika wa elimu ya vipimo vya mizani kutoka mkoa wa Iringa Bw. Mwalubandu akifuatilia jambo kwa ukaribu zaidi.


Mwenyekiti wa TCCIA Wilaya ya Ludewa Bw. Charles Mwasanga akifuatilia mafunzo ya elimu ya matumizi ya vipimo vya mizani Wilayani humo


 Diwani wa Kata ya Ludewa Bi. Monica Mchilo akichangia madhara ya vipimo vya mabede, Plastiki na Ndoo.


Picha ya pamoja ya wafanyabiashara wa MATAMBA wilaya ya Makete, wakiwa na wawezeshaji wa TCCIA na wanahabari.


 Picha ya pamoja ya wafanyabiashara wa Wilaya ya Ludewa, wakiwa na wawezeshaji wa TCCIA na wanahabari.


Picha ya pamoja ya wafanyabiashara wa UWEMBA Wilayani Njombe wakiwa na wawezeshaji wa TCCIA na wanahabari.


Picha ya pamoja ya wafanyabiashara wa BULONGWA wilaya ya Makete, wakiwa na wawezeshaji wa TCCIA na wanahabari.


Baadhi ya wafanyabiashara wakifuatilia somo la madhara ya kutotumia vipimo vya mizani katika uununuzi na uuzaji wa mazao.

CHAMA cha wenye viwanda na wafanyabiashara Tanzania mkoa wa Iringa TCCI , kimewataka wafanyabiashara wote wa mazao kuacha mara moja mazoea ya kutumia vipimo visivyo vya kitaalamu katika ununuzi wa mazao kwa wakulima,  kwa kuwa hatua hiyo ni uvunjaji wa sheria ya mizani ya mwaka 1982., na badala yake watumia vipimo vya mizani. 

Hatua hiyo imekuja hivi karibuni baada ya TCCIA mkoa wa Iringa kuwakutanisha wafanyabiashara na wanunuzi wa mazao ili kuwapa elimu itokanayo na madhara ya kununua na kuuza mazao kwa kutumia vipimo visivyo rasmi kama NDOO, PLASTIKI na MADEBE jambo ambalo linchangia kudumaza uchumi wa wakulim na Taifa kwa ujumla.

Mafunzo hayo ambayo yamewafikia wafanyabiashara wa wilaya ya Ludewa, Makete na Njombe ymeonyesha dhahili namna wananchi wasivyo na ufhamu juu ya vipimo vya mizani, ambapo lawama kubwa zilielekezwa katika idara ya vipimo, kwa kushindwa kufika vijijini kukagua mizani hata inayotumika katika maduni na hivyo wananchi kupoteza imani na mizani hiyo.

Tanzania chamber of Commerce (TCCIA) mkoa wa  Iringa kupitia uongozi wake umewataka wafanyabiashara kuacha kuwaonea wakulima kwa kununua mazao yao kwa njia ya ujazo na hatimaye sasa watumie vipimo vya mizani.


Wananchi hao walisema hawana mazoea ya kutumia vipimo vya mizani kutokana na kutopatikana kwa vipimo hivyo, ikiwa pamoja na kupoteza imani kwa baadhi ya mizani ya wafanyabiashara, kutokana na wakaguzi kutofika katika Wilaya zao kufanya ukaguzi na hivyo kujikuta wakipunjwa katika manunuzi ya bidhaa yanyotumia mizani.

 Fikiria Nyambo mkulima wa Matamba Wilyani Makete alisema wamekuwa na mazoea ya kununua na kuuza mazao ya chakula kwa kutumia bede au plastiki jambo ambalo halina utaalamu.

“Unakuta hta katika soko la Chimala, tukifika na mazao pale wanatutaka tuanze kupima upya kwa mujibu wa mnunuzi, wengine wanataka gunia liwe na ujazo wa debe 8, wengine 9 hadi 10, sasa tukisema sisi tusiweke Lumbesa tunajisumbua, kwani huko tunakokwenda kuuza wanakataa,” Alisema

Greyson Buha alisema endapo serikali itahimiza kila mununuzi kuwa na mzani tatizo hilo litakwisha na kuwainua wakulima katika kilimo chao ambacho wamekuwa wakitumia gharamaa kubwa na kujikuta wakipata hasara wakati wa mauzo.

Witness Mwinuka alisema wamekuwa wakipata hasara pindi wafikapo na mazao katika masoko makubwa, kwani wafanyabiashara huwalazimisha kujaza upya katika magunia, na hivyo gunia moja kujaza debe zaidi ya 9 hadi kumi.

Juditha Mpoma mnunuzi wa mazao wa kijiji cha Bulongwa Wilayani makete alisema tatizo kubwa ni kukosekana kwa elimu juu ya matumizi ya mizani ni moja ya sababu kubwa ya matumizi ya madebe na ndoo katika upimaji wa mazao.

Naye Charles Mwasanga, mwenyekiti wa wafanyabiashara Wilaya ya Ludewa alisema tatizo kubwa linalowakabili wakulima wilayani humo ni ubovu wa miundombinu ya barabara, ambapo huwafanya wakulima wauze mazao yao kwa gharama ndogo pindi wanunuzi wanapofika Wilayani humo.


Wananchi hao walisema hujikuta wakilazimishwa kujaza mazao katika mifuko (Maroba) yenye kilo 200 kwa malipo ya ujazo wa kilo 100 hatua ambayo inarudisha nyumba uchumi wao.

“Gunia moja linalotakiwa kuwa na kilo 100, tunaliuza kwa ujazo wa kg 150 hadi 200, kilo 100 nzima tunadhurumiwa, sasa unadhani kama mfanyabiashara anahitaji gunia 100 amedhurumu kiasi gani, ni zaidi ya gunia 100 anajipatia bure, sasa kwa Wilaya nzima kuna hasara kiasi gani tunaipata,”? Alisema Mwasanga.


Mshauri mwezeshaji wa TCCIA mkoa wa Iringa Dustun Mpangala alisema endapo serikali haitaingilia kati katika kudhibiti ujazo huo wa lumbesa, kilimo kitashindwa kuwa mkombozi wa mkulima, kwani hatua  hiyo inadumaza nguvu kazi ya mkulima, na kuwa ni ukiukwaji wa sheria ya vipimo ya mwaka 1982.

“Ndugu zangu, kutumia vipimo vya madebe na ndoo ni ukiukwaji wa sheria ya vipimo ya mwaka 1982, na hakuna kitu kizuri kama kufuata sheria, kwani adhabu ya uvunjaji wa sheria, adhabu yake ni kubwa, fuateni sheria jamani,” Alisema Mpangala.

Hata hivyo makamu mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Iringa, Henry Mangenya alizishauri Halmashauri zote kuweka vipimo vya mizani katika masoko, ili kuwawezesha wakulima kutumia vipimo sahihi katika uuzaji wa mazao yao, na kuachana na mazoea ya kutumia ujazo wa vifaa visivyo rasmi, lengo likiwa ni  kuwaepusha wakulima kupata hasara inayochangia hata uchumi wa Taifa kudumaa.

MWISHO





No comments:

Post a Comment