Marehemu Daud Mwangosi akivishwa Skafu na mmiliki wa mtandao huu, Bi. Oliver Motto, ambaye ni mwanahabari aliyekuwepo katika tukio hilo la kuuawa Daud Mwangosi, Marehemu alivishwa skafu hiyo Siku ya maandamano ya UHURU WA VYOMBO VYA HABARI.
Marehemu Mwangosi, nayeonekana mguu wenye suruali ya Kaki, akiwa ameelekezewa mtutu ambao alifyatuliwa sekunde chache na kupoteza maisha yake, ktika kijiji cha Nyololo mkoani Iringa.
Marehemu Mwangosi, Kulia aliyenyanyua Kamera, akiwa katika kituo cha Kwanza cha ufunguzi wa Matawi ya CHADEMA dakika chache kabla ya kumfika umauti katika ofisi ya CHADEMA Nyololo, baada ya kutoka katika tawi hili la Kwanza lililofunguliwa.
Marehemu Mwangosi wa pili kulia, ambaye alikuwa mwenyekiti wa clab ya wanahabari mkoa wa Iringa (IPC) akiwa na wanahabari wenzie katika ziara ya kikazi katika Hifadhi ya Ruaha mkoani Iringa, mwenye Tshirt ya Orange ni katibu wa clab ya wanahabari mkoa wa Iringa (IPC) Bw. Frenk Leonard, akieleza jambo.
Marehemu Mwangosi akiwa ameshika bango siku ya UHURU WA VYOMBO VYA HABARI, akiwa na diwani wa Miyomboni/Kitanzini, Mh. Jesca Msambatavangu, katika mndamano ya siku hiyo.
WAKATI kamati ya Waziri wa mambo ya Ndani Mh,
Emanuel Nchimbi, ikiwa imetoa ripot yake
juu ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Chanel Ten, mkoa wa Iringa,
Marehemu Daud Mwangosi, aliyeuawa Septemba 2 katika kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, wakati akitimiza wajibu
wa kazi yake ya uandishi, nae mtuhumiwa wa
kesi hiyo ameshindwa kufikishwa mahakamani.
No comments:
Post a Comment