Friday, November 16, 2012

MAPADRE WAPIGWA RISASI, WALAZWA HOI


Padre Anjelo Bargio, paroko wa kanisa Kathoriki, parokia ya Isimani Iringa, ambaye amelazwa katika Hospitalia ya mkoa bada ya kuvamiwa na majambazi na kupigwa Risasi ya kifua, upande wa kushoto .
Hapa Paroko Anjelo akiwa mwenye furaha siku ya mahafali ya kidato cha nne katika sekondari ya Isimani.

IKIWA imepita siku moja tangu watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuvamia kanisa Kathoriki mkoani Iringa jimbo la Kihesa na kuiba baadhi ya mali, tena kanisa hilo hilo katika jimbo la Isimani mkoani Iringa, limevamiwa huku mapadre wakiumizwa vibaya.

Tukio hilo ambalo limetokea usiku wa kuamkia jana (Leo) ambapo majambazi waliingia katika kanisa hilo kwa kuvunja milango na kuwapiga risasi na panga padre Anjelo Bargio na Helmani Myala na kuiba fedha zaidi ya shilingi milioni 3.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema majambazi hao baada ya kuingia ndani walimkamata makamu wa Paroko na kumpiga wakitaka waonyeshwe kwa paroko huku wakidai wapatiwe fedha, na tukio hilo limetokea majira ya sa tano na nusu usiku.

Akizungumzia hali ya wagonjwa hao, kaimu mganga mkuu wa Hospitalia ya mkoa wa Iringa Dr. Haustin Gwanchele amesema wamepokea majeruhi watatu, mmoja akiwa ni mlinzi wa kanisa kathoriki Kihesa Bw. Bathromeo Nzigilwa ambaye alipigwa nondo kichwani na kupoteza fahamu nab ado mgonjwa huyo hajitambui.

Dr Gwanchele  amesema Nzigilwa ameumia maeneo ya kisogoni na hali yake siyo nzuri, huku siku ya leo(jana) wakiwamepokea wagonjwa wawili , kutoka kanisa katholiki parokia ya Isimani katika Wilaya ya Iringa.

Amesema amempokea padre Helmani Myala (36) ambaye amepigwa nondo na padre Anjelo Bargio (60) muitaliano ambaye naye alipigwa risasi kifuani upande wa kushoto na kutokea kulia, huku nyingine zikiwa bado mwilini na wanafanya mpango wa kuzitoa.

Mashuhuda hao wamesema majambazi walikuwa 7, huku wawili wakiwa na bunduki na waliobaki wakiwa na nondo na panga n kuwa wameiba zaidi ya shilingi milioni 3.

Hata hivyo wananchi wameiomba serikali kufungua macho na masikio yake, katika kulitatua tatizo hilo ambalo linaweza kuleta madhara makubwa kama halitatafutiwa ufumbuzi mapema, kwani  wanahisi kuwa ni mpango ulioratibiwa ili kulihujumu kanisa Kathoriki.

Kauli hiyo inakuja baada ya kanisa hilo katika mkoa wa Iringa, kuvamiwa mara tatu, huku awali kanisa katholiki Nyololo katika Wilaya ya Mufindi likivamiwa huku Padre akijeruhiwa vibaya, na majambazi wakiondoka na mali mbalimbali za kanisani hapo.

Huku katika Kanisa la jimbo kuu la Kihesa mkoani Iringa, majambazi hayo yamemjeruhi vibaya mlinzi na  kutoroka na fedha, huku wakifanya uharibifu mkubwa ikiwa pamoja na kuvunja baadhi ya mali kama Misalaba na kumwaga Sakrament.











No comments:

Post a Comment