Kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Iringa ASP Michael Kamuhanda, akitoa taarifa ya tukio la ajali Nyololo mkoani Iringa.
Bus aina ya Taqwa ambalo limepata ajali eneo la Nyololo mkoani Iringa.
Wananchi wakiangalia mabaki yatokanayo na ajali hiyo mbaya.
Bus aina ya Taqwa ambalo limepata ajali eneo la Nyololo mkoani Iringa.
Wananchi wakiangalia mabaki yatokanayo na ajali hiyo mbaya.
ABIRIA saba wamekufa papo hapo
baada ya basi la TAQWA waliokuwa wakisafiria kutoka jijini Dar es salaam kwenda
Mbeya kugongana uso kwa uso wakati gari aina ya Scania likitaka kulipita basi hilo.
Ajali hiyo ambayo imetokea jana
(juzi) majira ya saa kumi na moja jioni katika kijiji cha Nyololo Mufindi
katika Mkoa wa Iringa, imepoteza maisha ya watu hao saba akiwemo dereva na
utingo wake.
Akizungumzia ajali hiyo Kamanda wa
jeshi la polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda alisema tukio hilo lilitokea
katika barabara kuu ya Iringa na Mbeya ambapo gari namba TI04BZZ..T309 BTS
Scania mali ya Sogea Sotom mkazi Dar es salaam na lilikuwa likiendeshwa na Johanis
Udingo kabila Muhaya (32).
Kamuhanda alisema Gari hiyo ilikuwa
ikitaka kulipita basi la Taqwa lenye namba T 273 CBR Nissan lililokuwa
likiendeshwa na Abrahaman Abdul (32)
Mwarabu wa Ilala jijini Dar es salaam, na kusababisha kugongana uso kwa uso na
gari lenye namba T 597 AMZ / T227 AVKSC Scania mali ya Nyato Transipot
Ltd DSM iliyokuwa ikiendeshwa na dereva ambaye hakuweza kufahamika jin lake.
Akitaja majina ya watu waliokufa
katika ajali hiyo Kamuhanda alisema ni Abdalahman Abdul (32) Mwarabu ambaye ni
dereva wa basi, Nassoro Rashid Said (27) kabila mzigua wa Tanga ambaye alikuwa
ni Kondakta wa basi hilo.
Wengine ni Shasin Ramadhan Shaban
(32) fundi magari kabila Msambaa anayeishi Dar es salaam, Ally Suleiman (26) Mwarabu na mfanyabiashara wa
Dar es salaam, pamoja na abiria watatu ambao hawajafahamika majina yao.
Aidha Kamuhanda alisema pia ajali
hiyo imesababisha kujeruhiwa kwa abiria 25, wanaume wakiwa 16 na wanawake 9
ambao wote wamelazwa katika Hospitali ya Mafinga Wilayani Mufindi Iringa, na
kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.
Hata hivyo mganga mkuu wa Hospitali
ya Wilaya ya Mufindi Dr. Erick Bakuza
alisema walipokea majeruhi 44, wanaume wakiwa 27 na wanawake 17, huku akipokea maiti 7, kati yake Wanaume
wakiwa 6 na mwanamke mmoja.
Dr. Bakuza alisema kati ya majeruhi
hao 44 tayari majeruhi 3 wameruhusiwa na hivyo Hospitali kubaki na majeuhi 41, huku 3 wakiwa na hali mbaya na kufanyiwa
utaratibu wa kuwasafirisha katika Hospitali kubwa jijini Dar es salaam pamoja
na Hospitali ya Rufaa Iringa.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment