Eneo la uzinduzi wa mradi huo wa barabara.
Akiwa na viongozi mbalimbali eneo la uzinduzi wa mradi huo.
Akisalimiana na wananchi.
RAIS Jakaya Kikwete
ameziagiza mamlaka zote zinazosimamia ujenzi wa barabara, kutowafumbia macho watu wachache wanaokwamisha miradi hiyo kwa tamaa zao za fedha.
Rais Kikwete aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa jimbo la Isimani mkoani Iringa katika uzinduzi wa mradi wa barabara eneo la Migoli - Mtera alipofika kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Iringa - Dodoma.
Rais Kikwete alisema mamlaka zinazohusika zisipodhibiti wizi huo miradi ya ujenzi ukiwamo huo wa Iringa- Dodoma unaweza kukwama kutokana na udokozi wa mafuta, vipuri na alama za barabarani, na kuwa ili kutunza
barabara hizo ni vema wanaohujumu miundombinu wakafichuliwa na
kuchukuliwa hatua kali.
Hata hivyo alisema mbali
ya serikali kuendelea na uboreshaji wa miundo mbinu
hapa nchini bado anawataka watanzania kutambua jitihada
hizo .
Alisema kuwa sasa
watanzania wanaweza kusafiri hadi Kenya na Uganda kwa barabara ya
lami na kuwa bado jitihada zitaendelea daima.
Rais Kikwete
alisema kuwa mbali ya serikali kujipanga kwa
ujenzi wa barabara bado lengo la serikali ni kuhakikisha
nchi nzima inaunganishwa kwa mtandao wa barabara ya lami na
kuwa kazi hiyo tayari imeanza.
Alisema kuwa serikali
yake toka imeingia madarakani imeendelea kuongeza
fedha katika mfuko wa barabara na kuwa lengo ni
kuendelea kuongeza zaidi fedha katika mfuko huo ili
kuwezesha ujenzi wa barabara nchini kuweza kukamilika
Aliwapongeza viongozi wa TANROADS kwa kazi nzuri
wanayoendelea kuifanya na kwa mbali ya kupongezwa bado hawapaswi
kulewa sifa na badala yake kuendeleza jitihada za
kusimamia kazi hiyo kwani upo usemi unao sema kuwa mgema akisifiwa
pombe huweka maji .
Pia Rais Kikwete
alimpompongeza waziri wa fedha Dkt Wiliam Mgimwa kwa kuendelea
kuidhinisha fedha kwa ajili ya miradi ya barabara hapa nchini na
kuwa bila wizara hiyo kutenga bajeti kazi hiyo
ingeendelea kuwa ngumu.
Akizungumzia kuhusu amani na utulivu
nchini Rais Kikwete alisema wapo baadhi ya watu usiku
na mchana wamekuwa wakipanga mipango mibaya ya kuvuruga amani
ya nchi hii na hivyo noi vema watanzania kuwaepuka watu wenye
nia ya kuchafua nchi hii kwa kuchochea vurugu.
Alisema iwapo
watanzania watakataa kuwasikiliza watu hao wala kushirikiana nao
kamwe Tanzania haitaingia katika machafuko yanayopangwa na watu hao wasio
penda mema.
Akitoa taarifa ya
ujenzi wa barabara hiyo waziri wa ujenzi Dk. John Magufuli alisema
kuwa wizara yake haitasita kuwachukulia hatua makandarasi
ambao watashindwa kutekeleza mikataba yao kama ilivyo elekezwa.
Waziri Magufuli alisema kuwa
wizara yake chini ya Rais Kikwete itaendelea kusimamia
ujenzi wa barabara na kujenga kwa kiwango cha lami na kuwa
wale wanaopinga jitihada hizo waendelee kusubiri kuandamana
katika barabara zilizojengwa na serikali ya CCM.
Waziri Magufuli alisema kuwa ujenzi wa
barabara hiyo ya Iringa -Dodoma yenye urefu wa Km 260 itajengwa kwa
zaidi ya bilioni 232 fedha kutoka benki ya maendeleo Afrika (ADB) na serikali
ya Japani pamoja na serikali ya Tanzania.
Wakati huo huo
wafanyakazi na vibarua wanaofanya kazi katika kampuni hiyo ya
kichina inayotengeneza barabara ya eneo la Migoli katika
barabara hiyo ya Iringa - Dodoma nusuru wavurugu siku baada ya
kupaza sauti mbele ya Rais wakilalamikia fedha
kiduchu wanazo pata kwa siku kwa kufanya kazi katika kampuni hiyo.
Vibarua hao na
wafanyakazi walisikika wakipaza sauti wakati Rais Kikwete
akiaga kwa ajili ya kuelekea katika chakula cha mchana kuwa
wanapunjwa sana mishahara na kuomba kusaidia kupiganiwa ili kulipwa
kima cha chini cha mishahara ya serikali.
"Mheshimiwa Rais una
ondoka ila sisi wafanyakazi tunaomba kusikilizwa kilio chetu
....hawa wachina wanatufanyisha kazi kwa ujira mdogo sana mheshimiwa
tunaomba kusaidiwa ....walipaza sauti wafanyakazi na vibarua hao
ambao walikuwa wamesimama juu ya mashine zao za kazi"
Hata hivyo Rais Kikwete
hakuweza kujibu chochote juu ya madai hayo kutokana na
eneo hilo kutawaliwa na kelele nyingi za burudani.
MWISHO
No comments:
Post a Comment