Moja ya stakabadhi ya ushuru wa zao la Mpunga, ambapo gunia 80 zilitozwa shilingilaki moja na elfu 60.
Wakielekea ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, kuonana na Mkurugenzi.
Wamefika nje ya geti la ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa (Siasa ni Kilimo).
Ofisa habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa- Evaristo Myovela (Albino) kifanya mazungumzo na wakulima hao.
Baadhi ya wakulima wakiwa nje ya ofisi za wakala wa Vipimo mko wa Iringa, ndani ya uwanja wa Saba saba Manispaa ya Iringa.
HATIMAYE wakulima wa zao la Mpunga
mkoani Iringa wameandamana hadi katika ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya hiyo, wakilalamikia kupanda kwa gharama za ushuru wa zao hilo, kutoka
shilingi elfu moja hadi shilingi 2000.
Wakizungumzia hatua ya uamuzi huo
wakulima hao wamesema, wamechoshwa na kiwango kikubwa cha ushuru ambacho
kinadumaza hali ya uchumi wao, na kushindwa kujikwamua kiuchumi na hata kuhofia
kuingia katika shughuli ya kilimo hicho mwaka huu.
Deo Mbongo amesema na Anjerous
Lijuja wamesema wanaogopa hata kuvuna Mpunga msimu huo, kwani bei za kuuza sokoni
zimeshuka, huku gharama ya ushuru ikiongezeka kwa asilimia 100 na hivyo wao
kama wakulima kupata hasara.
“Kingine tunacholalamikia hii
serikali yetu ni juu ya kutaka tupunguze ujazo wa gunia, yaani mpunga uwe na
kilo 75 badala ya 100, wakati hapo tena ushuru wamepandisha kwa asilimia 100, sasa
hii inatuumiza sana,” Alisema Lijuja.
Agnes
Kutika amesema awali walikuwa wakilipa ushuru wa gunia moja kwa shilingi moja
(1000/=) na mwaka jana mwishoni ushuru huo umeongezwa hadi kufukia kiasi cha
shilingi elfu mbili (2000/=) huku Manispaa nao wakitaka shilingi mia tano kila
gunia moja baada ya kufika nao katika mashine.
“Hali
hii ni kutuumiza sisi wakulima, hakuna tunachokipata, unalima kwa gharama
kubwa, mbolea na pembejeo zote ni bei juu, lakini wakati wa mavuno tena
serikali inatukamua kisai cha kupoteza mitaji yote, sioni hata sababu ya kutangaza
eti “Kilimo Kwanza”, mimi hapa nilipo nina watoto wanaonitegemea pamoja na
watoto yatima ninaowalea, sasa kwa mfumo huu naona kabisa ninakwama, kwani hata
hela ya mkopo niliochukua kwa ajili ya kuendeshea kilimo cha Mpunga imekatika
zaidi ya shilingi laki tano,” Alisema Agnes.
Abdala
Luvanda fedha walizoendeshea shughuli za kilimo ni mikopo kutoka
katika taasisi za kifedha, na kuwa wao wakulima wapo hatarini kuingia katika
madeni na benki hizo kutokana na serikali kuruhusu kuingia kwa Mchele kutoka
nje ya nchi, jambo lililoporomosha bei za zaoa hilo sokoni.
Yohana Fungo amesema kuna haja
serikali ikakaa nao katika meza ya pamoja ili kuona hasara wanazopata kwa
kutozwa ushuru mkubwa usiozingatia jasho
la mkulima, kwani pasipo kufanya hivyo kilimo ambacho ndiyo tegemeo kuu la
wananchi walio wengi kitakwama.
Ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri
ya Wilaya ya Iringa kupitia ofisa habari wake Evaristo Myovela amesema watazungumza na wakulima hao, ili
kuona kama kuna sababu za kupunguza ushuru huo.
“Sisi kama serikali wananchi ndiyo
tegemeo letu, tutakaa nao hawa wakulima ili kusikiliza malalamiko yao, na kama
kuna haja ya kutekeleza ombi hili la kupunguza ushuru tutafanya hivyo,” Alisema
Myovela.
Hata hivyo wakulima hao walifunga
safari hadi katika ofisi ya wakala wa Vipimo mkoa wa Iringa, kujua sababu za kutaka
gunia la Mpunga kuwa na ujazo wa kilo 75 pekee badala ya kilo 100 za awali.
Akitoa ufafanuzi juu ya kupungua
kwa ujazo huo, meneja wa wakala wa vipimo
mkoa wa Iringa Samwel Kilyunguzi amesema hatua hiyo ni katika kupiga
vita Lumbesa, kwani ujazo mkubwa ni hasara kwa mkulima, mfanyabiashara,
serikali pamoja na wamiliki wa magari.
“Serikali inaingia hasara
kutengeneza barabara zinazoharibiwa na ujazo mkubwa wa mizigo katika magari,
lakini pia hata wamiliki wa magari nao wanapata hasara ya kuharika mapema magari
kwa kubebeshwa mizigo mikubwa kupita tani zinazotakiwa, wale Makuli wanaoshusha
na kupakia mizigo hiyo pia wanapoteza maisha kwa kujitwika mizigo mikubwa
kushinda uzito wao, na pia mkulima naye anapata hasara kwa kuuza ujazo mkubwa, kwa
hiyo tunapiga vita Lumbesa kwa lengo la kuepusha hasara kwa makundi hayo yote,”
Alisema Kilyunguzi.
Wakulima hao waliitaka Halmashauri hiyo kupunguza gharama za ushuru huo, kutoka shilingi elfu mbili hadi kufikia shilingi elfu moja, ili kuweza kumudu gharama nyingine na kuweza kujikwamua kiuchumi.
No comments:
Post a Comment