Wednesday, December 11, 2013

AMREF "VIJANA WAANGAMIA KWA KUKOSA ELIMU YA AFYA"


Mwezeshaji wa mafunzo ya "afya ya uzazi  kwa vijana" Meshack Mollel Kutoka shirika la utafiti wa dawa na tiba (AMREF) akitoa somo kwa kundi la wanahabari waliohudhuria mafunzo hayo ambayo yamefanyika Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine SUA mkoani Morogoro.

Mchambuzi wa Sera kutoka shirika la utafiti wa dawa na tiba (AMREF) Bw. Meshack Mollel akitoa mada juu ya uandishi wa habari za afya ya uzazi kwa vijana  kwa Waandishi wa habari na Wahariri kutoka mikoa ya Iringa,Njombe,Mbeya,Morogoro na Dar es Salaam katika  chuo cha Kilimo SUA  Morogoro.




Imeelezwa  kuwa hakuna mfumo maalum wa  upatikanaji wa taarifa za afya ya uzazi kwa vijana na kuwasababishia  kupata changamoto mbali mbali ikiwa ni pamoja na maambukizi ya virusi vya Ukimwi,mimba za utotoni na magonjwa ya zinaa.
Hayo yameelezwa na mchambuzi wa  sera katika shirika la utafiti  wa dawa na tiba (AMREF) Bw. Meshack Mollel  alipokuwa akizungumza katika semina ya siku tatu ilitolewa na shirika hilo kwa  waandishi wa habari  kuhusu   haki za afya ya uzazi kwa vijana inayofanyika katika  chuo cha kilimo SUA Mkoani  Morogoro.
 
Aidha amesema vijana wamekuwa hawana elimu sahihi ya afya ya uzazi, kutokana na kukosekana kwa vituo vya utoaji wa taarifa hizo, na hivyo baadhi ya o kujikuta wakipotoshwa kutoka katika vyanzo visivyo rasmi.
 
Amesema hata tatizo la mimba   kwa vijana walio na umri mdogo, linatokana na  baadhi yao kuikosa elimu hiyo muhimu, na baadhi yao wakipata maambukizi ya Virus vya Ukimwi, na hivyo nguvukazi kubwa ya Taifa kupotea.

Mollel amesema ipo haja kwa wadau vikiwemo  vyombo vya habari kujikita katika kutoa elimu hiyo ya afya ya uzazi kwa vijana ili iweze kuwakia vijana walio wengi, kwa madai kuwa kundi hilo ni robo tatu ya Watanzania.
 
Na kuwa mpango wa mradi huo ni kuwafikia vijana Laki moja, huku vijana 100 wasio sikia nao wakifikiwa  na mrdi huo kwa muda wa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2011 hadi 2014.
 
Hata hivyo waandishi hao wamelitaka shirika la AMREF kupitia mradi huo wa "Afya ya uzazi kwa vijana" kuona wakati umefika sasa mradi kuvitumia vyombo vya habari katika kutoa elimu hiyo, ikiwa pamoja na kuwawezesha waandishi kufika maeneo ya nje ya miji ambako ndiko kwenye tatizo hilo la kukosekana na elimu ya afya ya uzazi kwa Vijana.
 
MWISHO

No comments:

Post a Comment