Wednesday, December 25, 2013

WATOTO 20 WAZALIWA MKESHA X-MAS


 Mmoja wa watoto wachanga waliozaliwa katika siku ya mkesha wa Sikukuu ya Krismas mkoani Iringa.
 Baadhi ya akinamama waliojifungua watoto siku ya mkesha wa kuamkia sikukuu ya X-Maswakisikiliza ushauri kutoka kwa ofisa muuguzi kitengo cha chanjo.
 Baadhi ya akinamama waliojifungua watoto siku ya mkesha wa kuamkia sikukuu ya X-Mas wakisubiri kwa hamu kuruhusiwa kurudi nyumbani.
JUMLA ya watoto wachanga 20 wamezaliwa katika Hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa, katika mkesha wa sikukuu ya Krismas,  ambapo jamii imewataka wazazi kuwalea watoto hao ili wawe mtaji na mbegu bora ya Taifa.

Mmoja wa akinamama waliojifungua mkesha wa siku ya Krismas Bi. Paulina Mgwilanga amesema anayofuraha kupata mtoto katika siku yenye historia kubwa ya dunia, na kuwa furaha hiyo ataionyesha pia katika malezi ya mtoto wake huyo.

Naye Happy Fredy, mzazi aliyejifungua mtoto wa kiume amesema tayari ametoa jina kwa mtoto huyo ambaye amependekeza aitwe Immanuel, kutokana na jina hilo kuwa na maana ya “Mungu Pamoja nasi,” na kuwa hilo jina kwake linawakirisha kuzaliwa kwa Mwokozi Yesu Kristo.

Mariam Sabula- Afisa muuguzi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa amesema kati ya watoto 20 waliozaliwa katika siku ya mkesha wa Sikukuu ya Krismas 16 niwakiume na wane niwa kike.

“Katika Hospitali hii ya mkoa wa Iringa wanawake 20 wamejifungua watoto usiku wa mkesha wa sikukuu ya Krismas, ambapo watoto 16 niwakiume na wane niwakike, na tunachoshukuru nikuwa wazazi na watoto wote hali zao ni nzuri, hakuna aliya na hali mbaya,” Alisema Sabula.

Lakini katika kusherehekea siku hii ya X-Mas  jamii imetakiwa  kuacha desturi ya kutoa zawadi na misaada ya vyakula na vinywaji pekee,  na badala yake wajikite katika kusaidia masuala yenye tija hususani sekta ya elimu.

Rai hiyo imetolewa na mdau wa elimu Mathew Glory Nganyagwa mkazi wa Manispaa ya  Iringa, wakati akikabidhi  vifaa vya shule vyenye thamani ya shilingi Milioni nne kwa wanafunzi zaidi ya elfu tatu wa Kata ya Mseke iliyopo Wilaya ya Iringa, hiyo ikiwa ni sehemu yake ya kusherekea sikukuu ya X- Mas.

Nganyagwa amesema ipo haja kwa jamii kubadili mfumo uliozoeleka wa kutoa zawadi na misaada hasa katika msimu wa sikukuu, na hivyo kujikita katika utoaji wa zawadi na misaada inayolenga sekta ya elimu.

Akizungumzia lengo la msaada huo Mathew alisema dhamira ya msaada huo ni kuwapa msukumo wanafunzi kuipenda zaidi elimu,  kwa kutoa misaada ya vifaa vinavyounga mkono sekta hiyo muhimu, ikiwa pamoja na kuwakumbusha wananchi juu ya kuzikumbuka shule zenye uhitaji wa vipaumbele vyenye tija.

Aidha Mathew aliitaka jamii kuwekeza zaidi katika sekta hiyo ya elimu ili kutatua changamoto zinazowakabili walimu na wanafunzi shuleni, kwa madai baadhi ya changamoto hukwamisha jitihada ya upatikanaji wa elimu, ambapo pia ameitaka jamii  kuacha mfumo wa kuchangia   masuala yasiyo ya lazima.

“Nimeona wakati msimu huu wa sikukuu mahitaji ya watoto siyo vyakula na vinywaji  pekee, nikakumbuka kuwa kuna zawadi na msaada muhimu unaosahaulika kama zawadi ya mtoto, na  mimi kama mdau wa elimu nikaona nije kutoa vifaa hivi kwa watoto wanaotaraji kuanza darasa la kwanza na wale wa sekondari,” Alisema Mathew.

Mdau huyo wa elimu amekabidhi kwa kila mwanafunzi Madaftari matano, karamu mbili, mkebe kwa kila mwanafunzi, ikiwa pamoja na Chaki za kuandikia kwa shule zote zenye uhitaji wa vifaa hivyo.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kaning’ombe Mohamed Mchamba alisema anayo idadi kubwa ya wanafunzi yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi, ambao wengi wao wamekuwa wakikosa mahitaji muhimu ya shule.

“Ninao wanafunzi wengi Yatima na wanaoishi katika mazingira magumu, ambao baadhi yao hushindwa hata kuandika kutokana na kukosa vifaa kama madaftari na karamu, lakini msaada huu utawasaidia sana,” Alisema Mchamba.

Sakina Mwenda mwalimu wa shule ya msingi Makota alisema shule yake inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa Chaki, tatizo ambalo linasababisha walimu kushindwa kuandika kazi nyingi ubaoni baada ya kubaki na vipande tu vya Chaki.

Naye mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kaning’ombe Pascal Mnyifuna alisema msaada huo umekuja wakati muafaka, kwani wanafunzi wengi wamekuwa wakikosa vifaa vya shule baada ya wazazi na walezi wao kumaliza fedha katika shughuli za Kilimo na sikukuu za Krismas na mwaka mpya.

Mnyifuna alisema kijiji chake kina idadi kubwa ya watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi na magumu, kutokana na asilimia kubwa ya watoto kulelewa na bibi au babu zao, baada ya wazazi wao kukimbilia mjini kufanyakazi, huku walezi hao wakiwa hawana uwezo wa kumudu mahitaji ya wajukuu zao.

“Watoto wengi hapa unaowaona wanalelewa na bibi au babu zao, siyo kama mama zao walifariki, hapana, wapo mjini wanafanyakazi, kwa hiyo wazee walio wengi  hawana uwezo  wa kuwahudumia wajukuu wao, nah ii ni kutokana na maisha duni waliyonayo, msaada huu ni mkubwa sana na utasaidia sana kukabilia na changamoto wanayoipata wanafunzoi kwani baadhoi yao huwa wanakosa hata Karamu na madaftari ya kuandikia,” alisema Mnyifuna.

Hata hivyo mratibu wa elimu Kata ya Mseke Eleonora Mwakalundwa alisema shule zake zinachangamoto ya Chaki, licha ya kuwa serikali imekuwa ikijitahidi katika kutatua tatizo hilo kwa kuwashirikisha na wananchi.

Mwakalundwa aaliitaka jamii pia kuiga mfano huo wa uchangiaji wa masuala ya elimu, ikiwa pamoja na wananchi kuacha imani potofu ya kuwaona wanaochangia kuwa ni watu wenye kipato kikubwa, huku baadhi yao wakidiliki kuwaita Freemason.

“Ninajua hapa kumekuwa na tabia ya zamani sana, mtu anapochangia mmekuwa mkimpa majina mengi na mabaya mara Freemason, na wengine hata wakiwakataza ndugu na jamaa zao wasijitolee kwa imani ya kulogwa, hayo ni mambo ambayo yamepitwa sana na wakati, tubadilike na kuona jukumu la uchangiaji wa masuala ya elimu ni yetu sote,” Alisema Mwakalundwa.



MWISHO



No comments:

Post a Comment