Saturday, December 29, 2012

NJAA YASABABISHA WANANCHI KUKIMBIA FAMILIA ZAO



 Wakulima wakiendesha shughuli ya kilimo kwa kutumia zana duni za jembe la mkono, ambazo hazina tija kwao.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri mkuu - Sera na Uratibu wa Bunge, Mh. Willium Lukuvi, ambaye pia ni mbunge wa jimbo hilo la Isimani, akisaini kitabu cha wageni katika jijiji cha Izazi, kabla ya kupata taarifa za janga la njaa kutoka kwa wananchi.
 Baadhi ya viongozi wa Kata ya Izazi na Migori katika Wilaya ya Iringa, Wakiwa katika kikao chao na Mbunge wao Mh. Willium Lukuvi, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri mkuu - Sera na Uratibu wa Bunge.  

WANANCHI wa Tarafa ya Isimani katika Wilaya ya Iringa, wamekumbwa na baa la njaa, na kusababisha baadhi yao kukimbia familia, .

Wakizungumzia hali hiyo katika kikao chao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri mkuu - Sera na Uratibu wa Bunge, Willium Lukuvi, ambaye pia ni mbunge wa jimbo hilo la Isimani,  Wananchi wa Kata ya Izazi walisema hali ya njaa imewaathiri zaidi, kwani baadhi ya wazazi na walezi wamekimbia familia zao.

Jasmini Muhalu mkazi wa kijiji cha Mnadani, alisema licha ya uwepo wa tatizo hilo, pia hata chakula kimekuwa hakipatikani kwa uraisi na hivyo kununu kwa gharama kubwa, huku bdhi ya wanaume wakikimbia familia zao na asilimia kubwa ya wakazi kijijini hapo kubaki wanawake na watoto.

“Yaani kungekuwa na njaa halafu chakula madukani kinapatikana haingekuwa tatizo kubwa sana, lakini sasa hata upatikanaji wa chakula umekuwa ni mgumu, mfano unga kilo moja unauzwa shilingi elfu moja na miambili, na debe moja shilingi elfu kumi na mbili, na hapa hakuna shughuli zozote za kiuchumi zaidi ya uvuvi ambao umeseimama kutokana na Bwawa la Mtera kukauka maji,” Alisema Jasmin

Eudia Masi mkazi kijiji cha Mnadani alisema hali ya njaa ni kubwa, kwani imesababisha baadhi ya wanaume kuhama makazi yao wakifuata maji katika Bwawa la Mtera kwa ajili ya kuendesha  shughuli za uvuvi ambazo nazo zimekuwa ni ngumu kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa katika bwawa hilo.

Petro Ng’ala alisema watu wamehama makazi yao ili kutafuta chakula katika maeneo mengine, na hivyo familia zilizoachwa kuishi maisha magumu, huku wanafunzi wakishindwa kuhudhuria masomo.

“Tumekuwa na idadi kubwa ya wanawake wanaoishi bila wanaume, kutokana na waume zao kukimbia kijijini hapa kwenda kutafuta ridhiki, lakini hali halisi ni mbaya zaidi,” Alisema Ng’ala.

 Costantino Makala mwenyekiti kijiji cha Mnadani alisema debe moja la mahindi katika kijiji hicho linauzwa shilingi elfu kumi n mbili, na hivyo familia nyingi kushindwa kumudu gharama hizo.

“Hali halisi ya chakula katika kijiji change ni shida sana, ni muda mfrefu sasa, na hili linatokana na mvua kushindwa kunyesha na hivyo kusababisha kukosa mavuno, kwa siku wanapata mlo mmoja, na hivyo wengi wameshindwa kuvulimia hali hii na kukimbia,” Alisema Makala.

Alisema hali hiyo imesababisha hata shughuli za maendeleo kukwama, kutokana na nguvu kazi ambayo ni wanaume walio wengi kuhama makazi katika kijiji hicho na kubaki wanawake na watoto.

Makamu mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Mnadani katika Kata ya Izazi Joyce Mgongolwa alisema hali hiyo imeathiri pia mahudhurio ya wanafunzi, kwani wengi hawafiki shuleni kutokana na asilimia kubwa ya wazazi kuwafanya ni wakuu wa kaya, kwa kuwaachia nyumba.

 “Mahudhulio kwa keli hasa kwa wale wasio na mitihani ilikuwa ni hali mbaya, wanafunzi hawafiki shule labda kwa yale madarasa yenye mitihani, nao utawaonea huruma, hasa ukifika muda wa mchana,” Alisema Mwalimu Mgongolwa.

Ofisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Lucy Nyalu, alisema tathmini imefanyika na kuonyesha uwepo wa tatizo hilo, na tayari wameomba  chakula  cha msaada katika ofisi ya waziri mkuu kitengo cha maafa.

Nyalu alisema tathimini ilionyesha upungufu wa chakula utakuwa mkubwa hasa mwezi wa kumi na mbili, na tayari Halmashauri wameomba tani miatano ili kuwasaidia wakulima hao chakula na hata kwa ajili ya kilimo.

Alisema Halmashauri inahimiza kitengo cha maafa ili kuwawezesha chakula wananchi hao, kwani asilimia kubwa ya wakazi hao hawana chakula na awali walikuwa wanategemea Bwawa la Mtera ambalo limekauka, huku zao la Mtama walilohimiza kulima limeshindwa kutoa mavuno kutokana na mvua kushindwa kunyesha kwa kiwango kinachotakiwa.

Hata hivyo Nyalu alisema tatizo la njaa limeongezeka zaidi baada ya mvua zilizoambatana na upepo mkali kufanya uharibifu katika maeneo hayo, huku vyakula vya wananchi hao vilivyohifadhiwa nyumbani mwao vikiharibiwa na mvua na hivyo tatizo la njaa kubwa zaidi.

MWISHO.




No comments:

Post a Comment