Saturday, December 8, 2012

WATU KUMI WAFARIKI KATIKA AJARI IRINGA


 Gari la Polisi likiwasiri katika Chumba cha kuhifadhia maiti mkoani Iringa, likiwa limebeba miili ya watu waliokufa katika ajari ya busi la Msanya, ambalo hufanya safari zake za Iringa kuelekea Usokami.
 Wananchi wa manispaa ya Iringa, wakipita kutambua miili ya marehemu waliokufa katika ajali iliyotokea katika kijiji cha Ihemi/ Kichakani mkoani Iringa

 Mmoja wa maiti akiingizwa katika chumba cha kuhifadhia maiti mkoani Iringa, baada ndugu zake kumtambua.

 Mmoja wa ndugu za marehemu akiwa amemtambua ndugu yake.



IKIWA imepita wiki moja tangu ajali mbaya ipoteza maisha ya watu 6 wa familia moja katika kijiji cha Tanangozi, ajali nyingine imeua watu zaidi ya 10 katika kijiji cha Kichakani katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Tukio hilo limetokea majira ya saa saba katika eneo la Ihemi kichakani, na kupoteza uhai wa watu 9 papo hapo huku majeruhi mmoja akifia Hospitalini.

Gari hilo aina ya Nisan lenye usajili namba T. 803 AJV mali ya kampuni ya Msanya lililokuwa likiendeshwa na dereva ambaye bado hajafahamika jina lake na amelazwa katika word namba 7.

Gari hilo limekuwa likifanya safari zake za Iringa kuelekea vijiji vya Mgama na Usokami, ambapo lilikuwa likitokea Iringa mjini kwenda Usokami.

Akizungumzia tukio hilo, kaimu mganga mfawidhi dr. Faustine Gwanchele alisema amepokea majeruhi 61, waliotibiwa na kuondoka ni 33 na waliolazwa ni 28.kati yao  wanaume 11 na wanawake 17.

Hata hivyo maiti watatu bado hawajatambuliwa, huku maiti saba zikitambuliwa na ndugu zao na kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya mkoa wa Iringa.

Kwa mujibu wa mashuhuda ajali hiyo ilitokea katika gati la mwisho katika barabara ambayo inaendelea kutengenezwa ambapo dereva alisimama katika gati hilo lilipinduka na kuingia kwenye korongoni.  

No comments:

Post a Comment