Sunday, January 6, 2013

KABATI-KATIBA STAR SEARCH YAMPATA MSHINDI


Mh. Ritta Kabati-Mbunge wa viti malumu CCM mkoa wa Iringa, akitoa nasaha kwa vijana walioshiriki tamasha hilo la Kabati Katiba Star Search.

 Mh. Ritta Kabati-Mbunge wa viti malumu CCM mkoa wa Iringa, (wa pili kushoto) akishiriki uimbaji.
 Kulia- Ni mkurugenzi wa Mnispaa ya Iringa Bi. Teresia Mahongo, akitazama awasanii wakiwajibika jukwaani(hawapo pichani).
 Msanii Alfred Mdembwe akitimiza wajibu wake.


 Mbunge Ritta Kabati akisubiri ugeni kutoka ofisi mbalimbali mkoani Iringa, ambao walifika katika tamasha hilo kumuunga mkono juu ya kile alichokifanya kwa vijana.
 Kamisaa Temmy Mahondo (mwenye Tshirt Nyeusi) akiwa na mratibu wa tamasha hilo la "Kabati katiba star search" Bw. Eddo Bashir.
 Wadau wa tamasha hilo wakisubiri kumpata kinara wa mashindano hayo yaliyowashirikisha wasanii 400 wa muziki wa kizazi kipya mjini Iringa.

 Msanii Naomi Mgima, akijiandaa kuingia katika ukumbi wa Twisters kushuhudia mpambano huo.
 Mh. Ritta Kabati, akitoa taarifa ya mpango huo na malengo yake.
 Mkuu wa mkoa wa Iringa  Dr. Christine Ishengoma ambaye alikuwa mgeni rasmi, akisoma hotum juu ya sanaa na wasanii kuwa mfano bora wa kuigwa katika jamaii.
 Mbunge Ritta Kabati, akisikiliza jambo kwa makini.


 MC-(Master of  Sermon) wa shughuli hiyo Bw. Denis Mlowe, akiwajibika vilivyo Stegin.


Mratibu wa shindano hilo, Bw. Eddo Bashir akiwatangaza washindi wa Kabti Katiba Star Search.
Msanii Emanuel Mgata (wa kwanza kulia) aliyeshika cheti ndiye aliyeibuka mshindi wa nafasi ya kwanza wa shindano la Kabati Katiba Star Search, akiwa amesimama na mkurugenzi wa mashindano hayo Mbunge Ritta Kabati.

WASANII wa tasnia mbalimbali nchini wametakiwa kuacha mara moja kuiga mitindo ya kimagharibi ambayo haiendani na maadili ya kitanzania ambapo hujikuta wakitengwa na jamii.

Wito huo umetolewa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Flavor) wa mjini Iringa, wakati wa kumsaka mshindi wa shindano la Kabati Katiba Star Search, lililoandaliwa na mbunge wa viti malumu mkoa wa Iringa Ritta Kabati, lililofanyika katika ukumbi wa Twisters mjini Iringa.

Wakizungumzia tabia za baadhi ya wasanii Nickson Sanga na  Naomi Mgima walisema kufanya mambo ya kuiga tabia za nchi nyingine, kunawafanya baadhi yao kutengwa na jamii na hivyo kushindwa kupokelewa kwa kazi zao na kupoteza fulsa hiyo ya ajira.

Nickson (DJ Nass) alisema endapo kundi la vijana wataitumia vema fulsa hiyo ya muziki na sanaa ya uigizaji pasipo kufanya masuala yasiyoipendeza jamii, sanaa hiyo inaweza kutoa ajira kubwa kwa kundi la vijana ambalo linakabiriwa na changamoto hiyo.


“Mimi ninawasihi vijana wenzangu, kwani ninaona muziki wa kizazi kipya unatusaidia kwa kutoa ajira kwa vijana nchini, lakini utumiaji wa dawa za kulevya ni katika mambo yanayoudumaza muziki  huu, na kufanya maadali yazidi  kumomonyoka,” Alisema Nickson.

Naomi alisema muziki huo na sanaa ya uigizaji ni moja tasnia ambazo zimeinua vijana wengi nchini lakini baadhi yao wamekuwa wakiitumia ndivyo sivyo, kwa kuiga mambo yasiyofaa, na hivyo kuonekana sanaa hiyo kama ni uhuni.

Aidha alisema changamoto kubwa inayowakabiri wasanii wa kike, ni pamoja na kukithiri kwa rushwa ya ngono katika hatua wanazopitia za kufanikisha muziki wao uweze kusikika.

“Sioni kama kuna sababu ya kuwa msanii mpaka ufanye mambo ya kuishangaza jamii, unajua sisi ni kioo cha jamii, sasa inatupasa tufanye yale yanayoifunza jamii, na watu waige mambo mazuri kutoka kwetu, kuvaa nusu uchi siyo ndiyo usanii, huo ni ulimbukeni tu, tena kibaya zaidi baadhi yetu tunajikuta tukiingia hadi katika matumizi ya dawa za kulevya, kuna haja ya kuachana na masuala hayo yasiyofaa ili tuwe walimu wazuri katika jamii yetu ya kitanzania, Alisema Naomi.

Mkurugenzi wa tamasha hilo mbunge Ritta Kabati, alisema lengo kuu la mashindano ayo, ilikuwa ni kuwakusanya vijana na kuwapa elimu ya umuhimu wa kutoa maoni ya katiba, kwani asilimia kubwa walikuwa hawana auelewa huo.

Kabati alisema ili kuwapata vijana wengi alianza kwa kufanya mashindano hayo, kwani alitambua vijana wengi wanapenda muziki huo wa kizazi kipya na hivyo baada ya kufanikisha lengo huu, aliendelea na mashindano ya uimbaji.

Katika tamasha hilo la kumpata mshindi wa mashindano ya Kabati Katiba Star Search mjini Iringa , mgeni rasmi alikuwa mkuu wa mkoa wa Iringa Dokta Christine Ishengoma ambaye aliwataka vija kuachana na desturi zisizofaa ambao zinachangia kuwapoteza.

Akizungumzia matatizo ya wasanii na mpango mzima wa shindano hilo, mkurugenzi wa Kabati Katiba Star Search, ambaye pia ni mbunge wa Viti maalumu CCM Ritta Kabati amesema lengo lilikuwa ni kutoa elimu ya umuhimu wa Katiba, na kutafuta vipaji vya vijana na kuviendeleza.

Dr. Ishengoma aliwasihi vijana  kuachana na  matumizi ya dawa za kulevya, ili waendane na jamii ya kitanzania ikiwa ni pamoja na kuinua vipaji vyao kwani muziki huo umekuwa ukisaidia kutoa ajira kubwa kwa vijana na hivyo kuachana na utegemezi kwa kukuza uchumi wa vijana.

Shindano hilo ni mara ya kwanza kufanyika, ambapo jumla ya vijana 400 walijitokeza katika mchakato wa awali ulichukua zaidi ya miezi miwili kuwachuja ili kupta vipaji vya muziki wa kizazi kipya, kwa lengo la kusaidia udhamini wa  kurekodi nyimbo na video.

Kwa mujibu wa mratibu wa mashindano hayo, kamisaa Temmy Mahondo na Muba msanii Emanuel Mgata aliweza kutangazwa kuwa ndiye mshindi wa kwanza kati ya wasanii 10 walioingia katika awamu ya tatu ya kumpata mshindi, na hivyo kupata fulsa ya kurekodiwa nyimbo zake bure, audio na video.

Kuna umuhimu viongozi wengine wakalikumbuka kundi hili la vijana, ambalo ndilo nguzo na nguvukazi ya Taifa, kwa kuwapa mafunzo mbalimbali, kulingana na uhitaji wao, ili kuwawezesha waweze kujitegemea na kupunguza mzigo mkubwa unaowakabiri wa ukosefu wa ajira.

MWISHO


No comments:

Post a Comment