Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Mh. Jesca Msambatavangu, ambaye pia ni diwani wa Kata ya Miyomboni/ Kitanzini, akitoa nasaha kwa wanafunzi wa kidato cha nne ambao matokeo yao ya mitihani hayakuwa mazuri, huku akiwasihi kuacha kukata tamaa.
Wanafunzio hao wakisikiliza kwa umakini mawazo mbadala baada ya kufeli mtihani wa kidato cha nne.
Wanafunzi hao wakiwa katika ukumbi wa Chuo kikuu cha Ruaha (RUCO) mkoani Iringa.
Mh. Jesca Msambatavangu (Katikati) akisisitiza jambo kwa wanafunzi hao, ambapo cha msingi amewataka vijana hao kutokata tamaa katika elimu, kwa matokeo hayo ya kidato cha nne, kulia ni Bi. Baby Baraka Chuma.
Mwanafunzi akiwaza jambo, katika ukumbi huo wa chuo kikuu cha Ruaha (RUCO).
Wanafunzi wakiwa katika viwanja vya chuo kikuu cha RUCO mkoani Iringa.
HATIMAYE
wanafunzi wa kidato cha nne waliopata matokeo mabaya ya mtihani wa Taifa, wa mwaka
2012 wamekutana kujadili mustakabari mzima wa nini kifanyike dhidi yao, ili kuokoa
ndoto zao ambazo zinadalili ya kuzima
ghafla, wakati wengine wakichukua uamuzi batili.
Mpango
huu ambao umeratibiwa na mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa,Bi- Jesca
Msambatavangu, na kufanyika katika chuo kikuu cha Ruaha-Ruco, lengo likiwa ni
kusikiliza vilio na simanzi za wanafunzi hao, ili kuwaonyesha njia mbadala ya
kufanya baada ya kupata matokeo hayo.
Wanafunzi
hao ambao wameonyesha nia ya uendelea na masomo, licha ya kuwa katika
sintofahamu ya kile kilichofanya matokeo yao kuwa mabaya, wamehudhuria mkutano
huo kwa wingi, huku wakiitaka serikali itambue kuwa yenyewe ndiyo chanzo cha
kuua ndoto zao za maisha.
Gerlady
Kiyeyeu aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya St. Michael ya Wilayani Kilolo amesema
serikali inatakiwa kufanya jitihada dhidi yao, ili kutopoteza ndoto za kundi
kubwa hilo la watanzania ambao ndiyo Taifa la baadaye, huku akiitaka serikali kuacha kuendeleza mgogolo na walimu.
“Serikali
yetu kwa matokeo haya inatakiwa, au irudie kusahihisha upya mitihani yetu, au
ituruhusu kurudia kidato cha nne pasipo na gharama ypyote, la sivyo itambue
kuwa inatupoteza kimsingi watanzania, na kuvunja mioyo ya wazazi wetu, ambao
kwa kiwango kikubwa wana hali duni,” Amesema Gerlady.
Naye
Upendo Vitus aliyekuwa mwanafunzi wa sekondari ya Tagamenda katika manispaa ya
Iringa, amesema matokeo hayo kwa kiwango kikubwa hana uhakika kama ni hyao,
kwani mtihani waliofanya ulikuwa wa kawaida na walikuwa na uhakika mkubwa wa
kufaulu.
“Kuna
baadhi yetu tulianza kufanya Tution ya kujiandaa na masomo ya kidato cha tano,
lakini tumeshtushwa sana na matokeo haya, mimi ninaiomba serikali iondoe
gharama za kulipia mtihani kwa sisi wote tunaorudia, ili kutupa nafasi wote,
tuweze kurisit,” Amesema Upendo.
Naye
Raphaely Mahenge, aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Iwawa Makete
mkoni Njombe, amesema hali duni ya wazazi wake itamfanya ashindwe kuendelea na
masomo, kwani tangu aanze kupata akili amekuwa akimuona mama yake akifanya biashara ya kuuza Makande.
“Mimi
niseme mama yangu ni mtu mwenye hali duni, sidhani kama nina uhakika wa
kujiendeleza katika shule binafsi na vituo hivi vya QT, kama shilingi elfu 20
alikuwa akilipa kwa awamu na kwa kusuasua, kutokana na biashara yake duni ya
Kande, atawezaje leo hii kunilipia ada ya kurisiti mtihani katika vituo
binafsi??, Amesema Raphaely.
Akizungumzia
mpango huo, mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Bi. Jesca Msambatavangu, amesema
lengo kuu ni kuwatia moyo vijana hao wasikate tama kutokana na matokeo hayo, na
pia kuwapa njia mbadala ya kujiendeleza katika vyuo vinavyotoa mafunzo na kozi
za muda mfupi, ili kuwa na sifa ya kujiunga na vyuo vikuu.
Bi.
Msambatavangu amewataka pia wazazi kuacha jazba dhidi ya vijana wao, kwani
hasira juu ya wanafunzi hao ndiyo sababu kuu inayochangia uwepo wa matukio ya
kujiua.
Naye
Bi. Baby Baraka Chuma, mkurugenzi wa kozi fupi na masomo endelevu, kutoka chuo
kikuu cha Ruaha(Ruco) amesema serikali iwaangalie kwa jicho la pili kwani
wanafunzi hao hawajafeli kwa kushindwa kujiandaa na mitihani yao, bali
waliwekeza licha ya kupata matokeo mbaya, na ndiyo sababu ya baadhi yao
kuchukua maamuzi ya kujitoa uhai.
Aidha
amesema kuna haja ya kujiuliza zaidi juu ya matokeo hayo na siyo kuwatupia lawama
zisizo na maana wanafunzi hao, huku akisisitiza serikali kusikiliza maombi ya
wanafunzi hao kurudia tena mtihani wa kidato cha nne pasipo na gharama.
“Mimi
nimepata picha baada ya kusikia mawazo ya hawa wanafunzi pamoja na matukio
yaliyojitokeza ya kujinyonga, kwani mwanafunzi ambaye hakufanya vizuri kwa
makusudi hawezi kuchukua uamuzi wowote akifeli, kwani anatambua wazi kuwa hakuonyesha
jitihada zozote, watoto hawa inaelekea walijiandaa vizuri na ndiyo maana wanaonyesha
jazba kwani kile walichokitaraji kimekuja tofauti” Amesema Baby.
Hata
hivyo wazazi nao wameonywa kuacha jazba na tabia ya ukali kwa wanafunzi ambao
wamepata matokeo mabaya, na kuwa huu ndiyo muda wa kuonyesha upendo dhidi ya
watoto wao, kutokana na janga walilolipata.
“Hakuna
haja ya kuwa mbogo kwa mtoto katika kipindi hiki kigumu, hapo ndiyo unaweza
kumsababishia matatizo mengine makubwa kama haya tunayoyasiki ya kujinyonga,
huu ni wakati mgumu kwa watoto hawa, na mzazi ndiyo anatakiwa kuonyesha upendo
wake wa dhati kwa kijana wake,”.
Hatua
ya kukaa na wanafunzi hao, ni mbinu mbada na sahihi ya kupata mawazo kutoka kwa
walengwa, juu ya nini kimefanyika, kuna haja ya masuala kama haya yenye maslahi
kwa Taifa ukafanyika uamuzi kama huu ambao umefanywa na Mh. Jesca Msambatavangu Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Iringa, ambaye pia ni diwani wa Kata ya Miyomboni Kitanzini.
MWISHO
No comments:
Post a Comment